Skip to main content

Ronaldo, Lieke Martens Wachezaji Bora Ulaya


Cristiano Ronaldo na Lieke Martens

NYON, Uswisi

MSHAMBULIAJI wa Real Madrid, Cristiano Ronaldoametajwa kuwa mchezaji bora wa Mwaka wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Ulaya (Uefa) akimshinda, Lionel Messi  na mlinda mlango wa Juventus, Gianluigi Buffon .

Ronaldo (32), aliisaidia Madrid kutwaa taji la Ligi ya Mabingwa kwa mara ya pili mfululizo na kumalzia kama mfungaji bora wa mashindano hayo akipachika mabao12.

Mreno huyo mwenye umri wa miaka 30 kwa sasa ameweka rekodi ya kutwaa tuzo hiyo mara tatu, akimzidi Messi mara moja.

Kwa wanawake mchezaji wa Barcelona ambaye ni raia wa Uholanzi mwenye umri wa miaka 24, Lieke Martens alitwaa tuzo ya mchezaji bora wa shirikisho hilo.

Martens aliisaidia nchi yake kutwaa ubingwa wa Ulaya katika majira haya ya joto na kutajwa mchezaji bora wa mashindano hayo.

Alimshinda mshambuliaji wa Wolfsburg,ernille Harder  na kiungo wa Lyon, Dzsenifer Marozsan .

Tuzo nyingine ijulikanayo kama 'President's Award' imetwaliwa na Francesco Totti, aliyestaafu soka Julai baada ya kuichezea timu ya Roma kwa miaka 24, ni mchezaji aliyeichezea timu moja tu.

Nyota huyo mwenye umri wa miaka 40 kwa sasa amepewa wadhifa wa Mkurugenzi wa klabu hiyo.

Tuzo  nyingine zilizotolewa kwa ajili ya Ligi ya Mabingwa 2016-17
Mlinda mlango bora : Gianluigi Buffon
Mlinzi bora:Sergio Ramos
Kiungo Bora: Luka Modric
Mshambuliaji Bora:Cristiano Ronaldo

Comments

Popular posts from this blog

Wachezaji waliosajiliwa na kuhama timu zote Ligi Kuu England

WAKATI dirisha la usajili Ulaya 2017 lililoanza Juni 9 lNdaniafungwa leo saa sita usiku, ifuatayo ni orodha ya wachezaji walioingia na kutoka katika timu 20 za Ligi Kuu England . Kama wewe ni shabiki wa moja ya timu hizo angalia orodha hii ujue wachezaji walioingia au kuondoka. ARSENAL Ndani Alexandre Lacazette - Lyon (ada haijatajwa), Sead Kolasac - Schalke(bure). Nje Wojciech Szczesny - Juventus, pauni 14m, Gabriel Paulista - Valencia, pauni 10m, Kieran Gibbs - West Brom, pauni 7m, Yaya Sanogo - ameachwa, Stefan O'Connor - ameachwa, Kristopher da Graca - ameachwa,Kostas Pileas - ameachwa, Takuma Asano - Stuttgart- mkopo Chris Willock - Benfica, (ada haijatajwa), Glen Kamara - ameachwa, Marc Bola - Bristol Rovers- mkopo Carl Jenkson - Birmgham- mkopo Cohen Bramall - Birmgham- mkopo Emiliano Martiez - Getafe-mkopo, Stephy Mavididi - Preston-mkopo, Ismael Bennacer - Empoli, (ada haijatajwa), Jon Toral - Hull, (ada haijatajwa). BOURNEMOUTH Ndani Asmir Begovic - Ch...

Zidane ajuta kumtwanga kichwa Materazzi

Picha mbili tofauti zinazomwonesha  Zinedine Zidane alipofanya tukio la kumpiga kichwa Marco Materazzi . MADRID, Hispania KOCHA wa timu ya  Real Madrid Zinedine Zidane amekumbuka tukio alilofanya kwa kumpiga kichwa aliyekuwa mlinzi wa timu ya taifa ya Italia,  Marco Materazzi katika kipindi chake cha mwisho cha uchezaji akisema kuwa hajisikii kujivuna kutokana na tukio hilo. Zidane alifanya tukio hilo wakati akiichezea Real Madrid, wakati akiitumikia Ufaransa katika mechi ya fainali ya kombe la Dunia 2006 ambayo iliisha kwa matokeo ya sare ya bao 1-1 kabla ya Azzuri kushinda kwa mikwaju ya penalti . Zidane ambaye alifanya mahojiano na kituo cha televisheni cha Ufaransa katika kipindi cha Telefoot na kuoneshwa kwenye runinga, alisema anajutia tukio hilo alilofanya katika siku za mwisho kama mchezaji. "Sijisikii kujivunia," Zidane alisema.  Zinedine Zidane akioneshwa kadi nyekundu kutokana na kumpiga kichwa  Marco Materazzi. "Sijivunii tuk...

Wazazi 'wamsusa' mpenzi wa Ronaldo mjamzito

Cristiano Ronaldo akiwa na Georgina Rodriguez na mtoto wao Ronaldo Jr MADRID, Hispania MPENZI wa Cristiano Ronaldo, Georgina Rodriguez anadaiwa kutengwa na wazazi wake. Mrembo huyo mwenye  umri wa miaka 23 anatarajia kujifungua mtoto wa kike Oktoba mwaka huu na kuongeza familia familia yake na Ronaldo inayokuwa kwa  haraka,  lakini kuna taarifa mama na baba yake hawajihusishi katika ujauzito huo. Kwa mujibu wa gazeti la Marca la Hispania, Rodriguez hamekuwan hana uhusiano mzuri na wazazi wake. Limeripoti kuwa kutokana na baba yeke Jorge Eduardo Rodriguez kuishi Argentina, na mama yake, Ana Maria Hernandez yuko nchini Italia, anamaliza kipindi chake cha ujauzito bila ya kupata sapoti. Mwanamitindo huyo mwenye damu mchanganyiko ya Kihispania na ki-Argentina mzaliwa wa Jaca kaskazini mashariki mwa Hispania, amebakia  katika nchi aliyozaliwa na sasa yuko na nyota wa Real Madrid ,anarajia kupata mtoto ambaye atakuwa wa nne kwa Ronaldo. Mtoto atakayemza...