![]() |
| Cristiano Ronaldo alipokuwa mahakamani nchini Hispania Jumatatu iliyopita. |
MADRID, Hispania
MSHAMBULIAJI nyota Real Madrid, Cristiano Ronaldo amekiri kuwa anataka kuondoka katika timu hiyo mabingwa wa Ligi Kuu ya Hispania na Ligi ya Mabingwa Ulaya na kurejea tena England.
Nyota huyo ametoa kauli hiyo mufa mfupi kabla ya timu yake kupambana na United katika mechi ya kuwania Kombe la Shirikisho la Mpira wa Miguu Ulaya UEFA (UEFA Super Cup).
Madridi ni mabingwa wa Ulaya huku United ni bingwa wa Ligi ya Europa.
Radio Cadena Ser ya Hispania imesema Ronaldo alisema hayo wiki hii katika mahakama kuu ya Hispania wakati alipokwenda kusikiliza kesi inayomkabili ya tuhuma za kukwepa kodi kiasi cha euro milioni 14.7 (zaidi ya sh. bilioni 38.7) kutokana na haki zake za matumizi ya picha zake kibiashara.
Kesi yake ilisikilizwa kwa faragha mbele ya jaji Monica Gomez Ferrer Jumatatu na haikuwa kitu cha kushangaza habari za kesi hiyo kuvuja kwa vyombo vya habari kutoka na umaarufu wa Ronaldo.
Cadena Ser imeripoti kuwa Ronaldo alimwambia jaji : ' Sikuwa na matatizo kama haya nilipokuwa England… Ndiyo maana ninapenda kurejea England.’
Ronaldo ameonekana kukasirika kutokana na kutuhumiwa kukwepa kodi na gazeti la ‘A Bola’ la Ureno limesema kuwa ameamua ataondoka Hispania kutokana na suala hilo.
Huku timu ya PSG ikimnyakua Neymar na Manchester United imekuwa ikihisi inaweza kumsaini tena mchezaji wao wa zamani Ronaldo.
Baada ya kusikilizwa shauri lake kwa dakika 90 katikati ya wiki, Ronaldo alionekana kuwa na wazo la kuondoka katika majira haya ya joto bado liko kichwani mwake.
Real Madrid iko tayari kuuza mmoja kati ya washambuliaji wake watatu, Karim Benzema, Ronaldo na Gareth Bale katika majira haya ya joto na ili kutoa nafasi kwa Kylian Mbappe (18) ambaye thamani yake inatajwa kuwa euro milioni 180 (zaidi ya sh. bilioni 474), ambaye amesema hataki kuhamia katika timu ambayo itamweka benchi.
want to come only to sit on the bench.

Comments
Post a Comment