MSHAMBULIAJI Cristiano Ronaldo amefanya mazoezi na wenzie pamoja na kwamba Shirikisho la Mpira wa Miguu Hispania limemfungia mechi tano kutokana na kosa la kumsukuma refa baada ya kuoneshwa kadi ya njano ya pili katika mchezo dhidi ya Barcelona .
Ameweka picha yake akiwa na wachezaji wenzie wa Instagram na kuandika maneno, 'Madrid timu ya ushindi.'
Katika mchezo huo wa kuwania Kombe la Hispania linalowaniwa na bingwa wa La Liga na Copa del Ray, Madrid ilishinda mabao 3-1, mchezo wa marudio utachezwa Jumatano hii katika Uwanja wa Santiago Bernabeu.
Barcelona ilipata kipigo cha mabao 3-1 huku ikiwa haina Neymar ambaye amehamia katika timu ya PSG.
Pia Messi na wachezaji wenzie wamerudi mazoezini leo wakijaribu kusahau kipigo walichopata, aliweka picha yao kwenye
Instagram, na kulaumu kipigo walichopata akisema kuwa ni kibaya, lakini maisha yazima yaendelee. Ndiyom kwanza yanaanza.
Ronaldo amefungiwa mechi tano la Ligi Kuu ya Hispania kutokana na kumsukuma refa baada ya kuoneshwa kadi ya njano ya pili kwa kile alichokiona kama alidanganya kwa kujiangusha katika eneo la penalti alipokuwa akikabana na Samuel Umtiti.
Pia ametozwa faini ya pauni 2,700 (zaidi ya sh. milioni 7.8 kwa tukio hilo la kumsukuma refa Ricardo de Burgos Bergoetxea .
"Kuvuta, kusukuma au kutingisha ya kufanya shambulio lolote dhidi ya wasimamizi wa mechi, hata kama ni ni vurugu ndogo bila ya kusababisha vurumai, itatolewa adhabu ya kufungiwa mechi kuanzia nne hadi 12," inasema kanuni kifungu cha 96.

Comments
Post a Comment