Skip to main content

Rais Fifa ampongeza Karia, amwalika Uswisi




Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Wallace Karia (kulia) akiwa na makamu wake Rais, Michael Wambura.

RAIS wa Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (Fifa), Gianni Infantino, ametuma salamu za pongezi kwa shirikisho la Tanzania (TFF), Wallace Karia kwa kuchaguliwa kuwa Rais wa TFF kwa kipindi cha miaka minne ijayo ya 2017-2021.
Taarifa ya TFF iliyotolewa na Ofisa habari wake, Alfred Lucas ilisema Infantino amempongeza Karia na viongozi wenngine kwa barua maalumu.
Katika barua yake hiyo ya Agosti 14, 2017 aliyoiandika kutoka Zurich, amesema: “Ningependa kuchukua nafasi hii kukupa pongezi zangu dhati. Nakutakia kila la kheri katika majukumu yako.”

Rais wa Fifa, Gianni Infantino
Amesema hana shaka na uwezo wa Karia hasa ikizingatiwa kuwa alikuwa Makamu wa Rais wa kipindi kilichopita, hivyo atakuwa fursa thabiti ya kuiletea nchi maendeleo ya mchezo soka.
“Kwa wakati wote, nakuhakikishia ushirikiano wa kutosha kutoka Fifa katika malengo yako. Milango ya Fifa iko wazi wakati wowote wewe kuja kujadili masuala ya mchezo wa mpira wa miguu hasa eneo la utawala.
“Ningependa kuchukua nafasi hii kukualika kuja hapa Zurich (Uswisi) wakati wowote kuanzia sasa ambako nitapata  fursa ya kukutambulisha maeneo mbalimbali ya Fifa. Nimeagiza upande wa utawala kuwasiliana nawe kuona na kupanga tarehe rasmi ya safari,” amesema na kuongeza:
“Nikutakie tena kheri na fanaka, nguvu na kila aina ya mafanikio katika majukumu yako mapya huku nikitarajia ujio wa kuonana nawe haraka.”
Wakati huo huo, Shirikisho la Mpira wa Miguu la Rwanda (FERWAFA) kupitia Rais wake,Nzamwita Vincent nalo kwa upande wake wamempongeza Rais wa TFF, Wallace Karia kwa kuchaguliwa kuwa kiongozi mpya wa shirikisho. 
FERWAFA imesema kwamba Rwanda itaendelea kuwa bega kwa bega na Tanzania katika maendeleo ya mpira wa miguu kwa ushirikiano baina ya nchi mbili kadhalika ukanda wa Afrika Mashariki unaounda Baraza la Sola la nchi za Afrika Mashariki.

Comments

Popular posts from this blog

Wachezaji waliosajiliwa na kuhama timu zote Ligi Kuu England

WAKATI dirisha la usajili Ulaya 2017 lililoanza Juni 9 lNdaniafungwa leo saa sita usiku, ifuatayo ni orodha ya wachezaji walioingia na kutoka katika timu 20 za Ligi Kuu England . Kama wewe ni shabiki wa moja ya timu hizo angalia orodha hii ujue wachezaji walioingia au kuondoka. ARSENAL Ndani Alexandre Lacazette - Lyon (ada haijatajwa), Sead Kolasac - Schalke(bure). Nje Wojciech Szczesny - Juventus, pauni 14m, Gabriel Paulista - Valencia, pauni 10m, Kieran Gibbs - West Brom, pauni 7m, Yaya Sanogo - ameachwa, Stefan O'Connor - ameachwa, Kristopher da Graca - ameachwa,Kostas Pileas - ameachwa, Takuma Asano - Stuttgart- mkopo Chris Willock - Benfica, (ada haijatajwa), Glen Kamara - ameachwa, Marc Bola - Bristol Rovers- mkopo Carl Jenkson - Birmgham- mkopo Cohen Bramall - Birmgham- mkopo Emiliano Martiez - Getafe-mkopo, Stephy Mavididi - Preston-mkopo, Ismael Bennacer - Empoli, (ada haijatajwa), Jon Toral - Hull, (ada haijatajwa). BOURNEMOUTH Ndani Asmir Begovic - Ch...

Zidane ajuta kumtwanga kichwa Materazzi

Picha mbili tofauti zinazomwonesha  Zinedine Zidane alipofanya tukio la kumpiga kichwa Marco Materazzi . MADRID, Hispania KOCHA wa timu ya  Real Madrid Zinedine Zidane amekumbuka tukio alilofanya kwa kumpiga kichwa aliyekuwa mlinzi wa timu ya taifa ya Italia,  Marco Materazzi katika kipindi chake cha mwisho cha uchezaji akisema kuwa hajisikii kujivuna kutokana na tukio hilo. Zidane alifanya tukio hilo wakati akiichezea Real Madrid, wakati akiitumikia Ufaransa katika mechi ya fainali ya kombe la Dunia 2006 ambayo iliisha kwa matokeo ya sare ya bao 1-1 kabla ya Azzuri kushinda kwa mikwaju ya penalti . Zidane ambaye alifanya mahojiano na kituo cha televisheni cha Ufaransa katika kipindi cha Telefoot na kuoneshwa kwenye runinga, alisema anajutia tukio hilo alilofanya katika siku za mwisho kama mchezaji. "Sijisikii kujivunia," Zidane alisema.  Zinedine Zidane akioneshwa kadi nyekundu kutokana na kumpiga kichwa  Marco Materazzi. "Sijivunii tuk...

Wazazi 'wamsusa' mpenzi wa Ronaldo mjamzito

Cristiano Ronaldo akiwa na Georgina Rodriguez na mtoto wao Ronaldo Jr MADRID, Hispania MPENZI wa Cristiano Ronaldo, Georgina Rodriguez anadaiwa kutengwa na wazazi wake. Mrembo huyo mwenye  umri wa miaka 23 anatarajia kujifungua mtoto wa kike Oktoba mwaka huu na kuongeza familia familia yake na Ronaldo inayokuwa kwa  haraka,  lakini kuna taarifa mama na baba yake hawajihusishi katika ujauzito huo. Kwa mujibu wa gazeti la Marca la Hispania, Rodriguez hamekuwan hana uhusiano mzuri na wazazi wake. Limeripoti kuwa kutokana na baba yeke Jorge Eduardo Rodriguez kuishi Argentina, na mama yake, Ana Maria Hernandez yuko nchini Italia, anamaliza kipindi chake cha ujauzito bila ya kupata sapoti. Mwanamitindo huyo mwenye damu mchanganyiko ya Kihispania na ki-Argentina mzaliwa wa Jaca kaskazini mashariki mwa Hispania, amebakia  katika nchi aliyozaliwa na sasa yuko na nyota wa Real Madrid ,anarajia kupata mtoto ambaye atakuwa wa nne kwa Ronaldo. Mtoto atakayemza...