![]() |
| Kylian Mbappe |
PARIS, Ufaransa
PARIS Saint Germany baada ya kumnasa Neymar Santos, sasa inahesabu saa kupata saini ya Kylian Mbappe kwa ada ya pauni milioni160 (zaidi ya sh. bilioni 464.7).
Real Madrid nayo imekuwa ikimtaka mshambulkiaji huyo kinda mwenye umri wa miaka 18 wa timu ya Monaco na timu ya taifa ya Ufaransa baada ya kung'ara katika msimu uliopita .
Lakini timu ya PSG inayomilikiwa na mfanyabiashara raia wa Qatari ndiyo inaonekana kushinda vita, wachezaji wa timu hiyo wameambiwa kuwa Mbappe anajiandaa kutambulishwa katika Uwanja wa Parc des Princes kabla ya Jumatatu.
Kama uhamisho huo utakamilika, PSG itakuwa imewanyakua wachezaji wawili kwa pauni milioni 360 (zaidi ya sh. trilioni moja), wakati ikitaka kuwa moja ya klabu kubwa za Ulaya .
Monaco imekuwa ikisema inataka kubakia na mchezaji huyo licha ya kutakiwa na Real.
Lakini baba yake Mbappe anatumaini Monaco itamruhusu mwanaye kuondoka katika majira haya ya joto badala ya kusubiri ipite miezi 12.
Kauli hiyo imewasha taa ya kijani PSG kuanza kufanya mazungumzo kuhusu uhamisho utakaohusisha fedha nyingi kwa mshambuliaji huyo, ina matumaini ya kukubaliana na kuwa iko tayari kutoa dau ambalo linafanana ofa ya Madrid.
![]() |
| Neymar Santos |
Mbappe ameshawishika kuhamia PSG baada ya kukutana na kocha wa timu hiyo, Unai Emery aliyemwambia atakuwa na nafasi ya kucheza katika kikosi cha kwanza msimu huu, pamoja na wamemsaini Neymar kutoka Nou Camp kwa da ya pauni milioni 198 (zaidi ya sh. bilioni 575).
PSG baada ya kumsaini Neymar kwa kuvunja mkataba wake kutoka Barcelona ilizua swali kama timu hiyo inafuata sheria ya Financial Fair Play ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Ulaya (UEFA) inayozitaka kutumia fedha kadiri inavyopata kwa kuuza wachezaji na si kutoka nje.
Uefa ilianzisha sheria hiyo mwaka, 2013 ikilenga kuzisaidia klabu kuepuka kuwa na madeni makubwa kwa kukopa fedha ili kuzitumia kwa kusajili na kuzuia wamiliki kuongezea fedha kwa klabu zao kwa ajili hiyo.
Katika msimu huu tayari PSG inaonekana inaweza kutumia pauni milioni 372.5, pia imem saini beki wa kushoto wa hispania, Yuri Berchiche (pauni milioni14.5) na raia wa Brazil anacheza beki ya kulia Dani Alves (bure) .
Real, kwa kumkosa Mbappe anayelipwa pauni 200,000 (zaidi ya sh. milioni 500) kwa wiki, ni pigo kwake na inaweza kufanya kuelekeza nguvu kwa mshambuliaji wa Chelsea, Eden Hazard.


Comments
Post a Comment