![]() |
Paulinho
|
BEIJING, China
MCHEZAJI José Paulo Bezerra Maciel Júnior maarufu kama Paulinho ameonesha kuwa shujaa wa ndani na nje ya uwanja alipokuwa katika Ligi Kuu ya China, kwa mujibu wa mfanyakazi wa Guanzhou
Kiungo huyo wa Brazil hivi karibu amefanya kitendo cha huruma kwa kumpatia dereva wake gari aina ya Mercedes na na vitu vingine kabla ya kuhamia Barcelona kwa ada ya pauni milioni
36.5, zaidi ya sh. bilioni 105.
Baada ya Paulinho kuondoka katika timu ya Evergrande, Liang Ke ambaye ni mfanyakazi wa klabu ya China aliyokuwa akiichezea, alitumia mtandao wa kijamii unaofanya kazi kama Facebook , Weibo kuonesha ukarimu wake.
Aliandika Paulinho alikuwa mcheshi akimsalimia kila mtu anayekutana naye sehemu ya kazi na kusaidia wengine wenye uhitaji.
'' Ni mtu asiyetaka kupokea fedha yoyote, badala yake anapenda kutoa, kwa mfano alitoa visikilizio vya redio vya kichwani(Beats headphones) na gari lake aina ya (Mercedes-Benz) kwa aliyekuwea dereva wake China.
Alisema hali ya kuwa na roho nzuri si kwamba imetokana na fedha nyingi alizokuwa akipata kwa mshahara wake mkubwa. Kuna watu wengi ambao ni tajiri kuliko Paulinho, lakini ni wachache ni wakarimu na wanaoweza kuwa upendo kama yeye.”
Liang ameelezea jinsi gani Paulinho alivyomleta daktari wa viungo kutoka Brazil ili aje kumtibia na kufanya ajisikie vizuri.
Alisema Paulinho alilipa ada ya tuisheni kwa mtoto wa daktari wa viungo baada ya kumwezesha kusoma katika shule ya kimataifa. Pia alilipia gharama matibabu za mtoto mmoja aliyefanyiwa upasuaji.
“Paulinho aliweza hata kulipia tiketi za ndege na malazi katika hoteli ya nyota tano kwa mtaalamu wake wa viungo na familia yake walipokuwa na mechi za ugenini,'' aliandika.
Mwisho Liang alieleza jinsi Paulinho alivyovaa beji iliyokuwa na maandishi ya ‘FORÇA CHAPE’ na rangi za jezi ya Chapecoense kwa siri kuonesha kusikitika kutokana ajali ya ndege ilitokea na kuua wacheza 19 wa timu hiyo kati ya abiria 71 Novemba mwaka jana nchini Colombia.
Alifanya hivyo baada ya kuomba kwa wasimamizi wa mechi na kukataliwa.

Comments
Post a Comment