WAKATI maadhinisho ya Tamasha la Simba yakifanyika leo, wachezaji Haruna Niyonzima na Emmanuel Okwi wamekuwa gumzo, kwa mashabiki na wengi wakitaka kwenda uwanjani kuwaona wakati wa utambulisho au watakavyokuwa wakicheza dhidi ya Rayon Spots ya Rwanda kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Mchezo huo utaanza saa 10 ikiwa ni baada ya kupambw ana matukio mbalimbali ya burudani ambayo yamepangwa kufanyika.
Katika tamasha la leo, Simba inayonolewa na Kocha, Mkuu Mcameroon Joseph Omog itatambulisha wachezaji wake wapya na wa zamani, pamoija najezi zitakazotumia na timu na mashabiki kwa msimu wa 2017-18.
'Mimi ni shabiki wa Yanga, lakini nitakwenda uwanja kumwona Niyonzima ambaye kuondoka kwake Jangwani kumeniuma lakini ninampenda kwa kuwa ni mchezaji mzuri,'' alisema Juma Hussein ambaye Mkazi wa Kimara.
''Mimi nitanunua jezi nyenye jina la Haruna Niyonzima kwa bei yoyote, kisha nitakwenda uwanjani kumwona na wachezaji wengine waliosajiliwa Simba akiwemo Okwi,'' alisema Peter Chaula mkazi wa Kinondoni.
Pia ashabiki wengi Dar es Salaam walionekana kwenye meza za kuuza magazeti na kutembelea mitandao kuona habari za Tamasha la Simba, huku katika mazungumza wengi walikuwa wakimzungumzia Niyonzima ambaye alitambulishwa rasmi kwa waandishi wa habari jana na leo atakuwepo Uwanja wa Taifa akiwa amevalia jezi za Simba kwa mara ya kwanza tangu alijiunge akitokea kwa mahasimu wao Yanga alikocheza kwa misimu sita akitoke APR ya Rwanda.
Kwa upande wa mchezaji mpya kutoka klabu ya Yanga, Haruna Niyonzima alisema hana maneno mengi mguu ndi utaongea.
"Sina maneno mengi kikubwa ni ushirikiano na mguu ndiyo utaongea, hivyo wapenzi waje kwa wingi kuangalia nini tunafanya wachezaji wao, "alisema Niyonzima.
Akizungumzia mchezo huo, Kocha Msaidizi wa klabu hiyo, Jackson Mayanja, alisema utakuwa wa tatu kwa kikosi chao ambacho kilicheza mechi mbili nchini Afrika Kusini.
Alisema kupitia mchezo huo wataangalia wachezaji wao wapya na wa zamani ikiwa ni shehemu ya maandalizi kabla ya kuanza kwa msimu huo.
"Tuna amini mchezo huu dhidi ya Rayon utatupa sura ya kikosi chezo kabla ya kuanza kwa msimu, tutatumia zaidi kuangalia kitu gani kinatakiwa kufanyika kabla ya msimu mya haujaanza,"alisema Mayanja.
Ciao...

Comments
Post a Comment