MADRID, Hispania
MSHAMBULIAJI wa Barcelona, Neymar Santos sasa inaonekana anahesebu saa kutua katika timu ya Paris St-Germain, baada ya kupewa ruhusa kwenda kufanya mazungumza na timu ya Paris St-Germain kuhusu uhamisho wake utakaovuja rekodi ya dunia kwa ada ya pauni milioni 198 (zaidi ya sh. bilioni 586).
Mchezaji huyo leo amewaambia wachezaji wenzie walipokuwa mazoezini kwamba ametakiwa kuondoka katika klabu hiyo ya Hispania.
Amepewa ruhusa na kocha wa Barca kocha Ernesto Valverde kutofanya mazoezi na kuangalia namba ya kushughulikia hatima yake ya baadaye.
Nyota huyo mwenye umri wa miaka 25 kwenye mkataba wake kuna kingele cha kuuvunja kwa pauni milioni 198 (zaidi ya sh. bilioni 586), kiasi ambacho PSG inadaiwa iko tayari kulipa.
Hatua hiyo imekuja baada ya Rais wa miamba hiyo ya La Liga, Javier Tebas katika mahojiano yake na Mundo Deportivo kusema watawachukulia hatua mabingwa wa zamani wa Ufaransa kwa kuwashtaki Fifa kama Shirikisho la Mpira wa Miguu la Ulaya halitachukua hatua.
Pia Rais wa PSG , Nasser Al-Khelaifi anajua kuhusa dhamira ya Barcelona.
Neymar alihamia Barcelona akitokea timu ya Santos ya Brazil mwaka 2013 kwa ada ya pauni milioni 48.6 (zaidi ya sh. bilioni 144) na kusaini mkataba wa miaka mitano mwaka 2016.
Wakala wake Wagner Ribeiro leo ameandika kwenye Twitter akiwa Paris, alisema mwaka jana mteja wake alipewa ofa ya kulipwa mshahara wa pauni 650,000 (zaidi ya sh, bilioni 1.9) bila ya kutosha kodi.
Pia alisehe nyota huyo ilibaki kidogo ajiunge na Manchester United.
Neymar amefunga mabao 105 tangu atue Barcelona, ameisaidia kutwaa makombe mawili ya Ligi Kuu vikombe vitatu vya Copas del Rey na Ligi ya Mabingwa.
Timu ya PSG inamilikiwa na kampuni ya Qatari Sports Investment (QSI) inayofanya biashara gesi asili ina jeuri ya fedha .

Comments
Post a Comment