![]() |
| Dk. Harrison Mwakyembe |
Mwandishi wetu
WAZIRI wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dk. Harrison Mwakyembe amewaambia wajumbe wa mkutano mkuu wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) wana dhamana kubwa ya kuchagua viongozi wazuri watakaosaidia kuleta maendeleo ya soka nchini.
Akizungumza wakati uzinduzi wa Mkutano Mkuu wa Uchaguzi mjini Dodoma leo, Mwakyembe amesema macho yote ya watanzania wapenda soka yameelekezwa kwa wajumbe wa 128 kutekeleza kazi kubwa ya katiba yao.
Mkutano huo utamchagua Rais wa Shirikisho, Makamu na wajumbe 13 wa Kamati ya Utendaji ya TFF watakaohudumia kwa miaka minne.
Amesema kama ilivyo kawaida ya chaguzi zote presha huwepo si tu kwa wagombea, pia kwa wapigakura lakini kwa nia njema ya kupata viongozi bora wa kuendesha chombo adhimu kwa ajili ya maendeleo ya soka nchini.
'' Ndugu wajumbe viongozi bora huibuliwa na wajumbe makini wanaoongozwa na dhamira njema, wasioyumbisha na vishawishi vya mpito, wanaongozwa na uzalendo.''
''Serikali inaamini katika mkutano huu kuna wajumbe makini wasioyumbishwa na vishawishi, wanaoongozwa na dhamira njema na uzalendo wa hali ya juu ambao wataibua viongozi bora wa TFF wenye ari, moyo, uelewa weledi na uadilifu unaotakiwa utakaosaidia kuipeleka soka katika hatua ya mbele,'' amesema Waziri Mwakyembe.
Amesema mafanikio huwa hayaji kwa maneno, kukamia bila ya kuwekeza na kujenga mazingira stahili, watanzania wanajua kuwa mpira ni mazoezi, ni nidhamu, ni afya, na ni ajira ya nguvu.
Mazingira hutengenezwa na vuiongozi makini tu wanaotambua thawabu ya uwajibikaji na kuheshinmu katiba, iliyowaingiza madarakani, wanaothamani uongozi wa pamoja.
Amesema kwa mara ya kwanza viongozi watakaochaguliwa wataapishwa mbele ya wapiga kura, kufuata sheria na kanuni kama vilivyo, wataapa kiapo cha utii mbele ya msajili.
Amesema kwenye mkutano huo kuna ugeni kutoka CAF (Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika) na Fifa) Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu), wajumbe wanatakiwa kuwaonesha kwa vitendo ukomavu wa kidemokrasia wa Tanzania katika uchaguzi duniani.
Amesema imepita miaka mingi hadi mwaka huu Tanzania imeshirikia mashindano ya Afcon kwa vijana umri chini ya miaka 17, Serengeti Boys. Pia mwaka huu Tanzania imefanya vizuri katika mashindano ya Cosafa kwa kushika nafasi ya tatu.
Amesema Tanzania inataka viongozi watakaolipeleka taifa mbali zaidi kimaendeleo, watakailea timu ya Serengeti Boys ambayo imepanda na kuwa ya chini ya umri wa miaka 21 Ngorongoro Boys ili kushiriki olipiki ya mwaka 2020 inatumia wachezaji wenye umri wa mika chini ya 23.
Wanatakiwa viongozi watakaoshirikiana na serikali kwa karibu kufanya maandalizi mazuri ya mashindano ya Afcon kwa vijana chini ya umri wa miaka 17 yanakaofanya mwaka 2019 nchini Tanzania kama wenyeji.
Amesema wanatakiwa viongozi watakaochaguliwa leo kuanza kazi mara moja ya kuiandaa timu ya Serengeti Boys mpya inayotoka na vijana walkiopatikana miaka miwi,li ilipita kwenye mashindano ya watoto wa chini ya miaka 13 ambao wamekusanywa na kuwekwa kwenye moja ya vituo michezo nchini.
Wanatakiwa viongozi ambao watashirikina na serikali kuwalea watoto wenye vipaji vya soka walioibuliwa kwenye mashindano ya karibuni ya Umisseta na Umitashumta yaliofanyika hivi karibuni.
'' Tunataka uongozi ambao unatambua na kusimamia kanuni ya Fifa ya Club Licensing kwa kujiamini kwani huo ni msingi wa mafanikio ya soka nchini.
''Serikali inataka uongozi ambao unatambua kuwa Fifa haikubatii rushwa, unatambua kwamba CAF haikumbatii rushwa na wala ubadhirifu kama ambavyo serikali haikubatii rushwa na ubadhirifu,'' amesema.

Comments
Post a Comment