![]() |
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo ,Dk Harisson Mwakyembe (watatu kulia) akimkabidhia bendera ya Taifa nahodha wa timu ya Taifa ya Riadha, Alphonce Simbu iliyoangwa Dar es Salaam jana kwenda London, Uingereza kushiriki mashindano dunia ya riadha yanayotarajiwa kuanza Ijumaa wiki hii.
Mwandishi wetu
TIMU ya taifa ya mchezo wa riadha imeagwa rasmina kukabidhiwa bendera ya taifa kabla ya safari ya ya kwenda kuiwakilisha nchi katika mashindano ya dunia yanatotarajiwa kufanyika London, Uingereza kuanzia Agosti 4 mwaka huu.
Timu hiyo yenye jumla ya wachezaji nane ilikabidhiwa bendera ya taifa jana na Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa, na Michezo Dr.Harrison Mwakyembe.
Akizungumza na waandishi wa habari, Waziri Mwakyembe alisema wizara serikali iko bega kwa bega na wadau wa michezo hapa nchini katika kuhakikisha kuwa sekta hiyo inapiga hatua.
“Kwanza kabisa nimetiwa moyo sana na ari ya vijana waliyonayo na kama mlivyoona na kusikia kwenye vyombo mbalimbali vya habari, vijana hawa wamepikwa vizuri na wana ari, moyo na uzalendo mkubwa na kilicho mbele yao ni kitu kimoja tu, kupambana kufa na kupona na kurudi na medali” alisema Waziri Mwakyembe.
“Tumeshazijua siri za wenzetu kufanikiwa katika riadha, mazoezi ndiyo kila kitu hata uvae hirizi ama utumie madawa huwezi kufanikiwa”.
“Unaposhinda medali unapandishiwa bendera na kupigiwa wimbo wa taifa hiyo ni heshima kubwa, vijana wangu tukimbie hata miguu ikifika kisogoni kimbieni”.
Rais wa Shirikisho la Riadha Tanzania (RT), Anthony Mtaka alisema mbali na jitihada kubwa zinazofanywa na chama hicho zipo changamoto nyingi ambazo zinahitaji nguvu za pamoja ili kuhakikisha kuwa riadha inaendelea mbele.
Amesema kuwa kwa kutambua hilo na kwa kutambua umuhimu wa wadau mbalimbali, wamekuwa wakifanya kazi kwa karibu sana na wadhamini (DStv) na majeshi mbalimbali kama vile JKT na JW ambapo wanariadha wengi wanatoka.
Jumla ya wanariadha wataoshiriki mbio ndefu za kilomita 42 ni, Alphonce Simbu mwenye rekodi ya 2:09.10 aliyo iweka hivi karibuni katika mashindano ya London Marathon, Ezekiel Jafari Ng’imba 2:11.55 aliyoiweka katika mashindano ya Hannover Marathon mwaka 2017.
Wengine ni Stephano Huche Gwandu 2:14.18 mashindano ya Tunis Marathon, Sara Ramadhani Mkera 2:33.08 akishinda katika mashindano ya Dusseldorf mwaka 2017 na Magdalena Crispin Shauri 2:33.28 akishinda katika mashindano ya Hamburg Marathon mwaka 2017.
Washiriki watatu waliosalia watakaoshiriki mbio fupi ni, Gerald Geay meta 5,000, Emmanuel Ginki Gisamoda meta 5,000 na Failuna Abdi Matanga akishiriki mbio za meta 10,000.
Mashindano ya dunia ya riadha yanatarajiwa kuanza Agosti 4 kuisha Agosti 13, mwaka huu.

Comments
Post a Comment