Skip to main content

Mwakalebela, Madega, Mayai waamsha dude urais TFF


Frederick Mwakalebela alipokuwa akizungumza na  waandishi wa habari (hawako pichani) Dar es Salaam leo
WAGOMBEA nafasi ya urais, katika uchaguzi Mkuu wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Frederick Mwakalebela, Iman Madega na Ally Mayai, wamezindua kampeni  na kuwataka wajumbe kuwachaga kuleta maendeleo ya mchezo huo.

Watatu hao wamefanya mikutano yao na waandishi wa habari, iliyofanyika leo jijini Dar es Salaam,  kila mmoja akiwashawishi wajumbe kuwapa nafasi ili kufanya vizuri katika uongozi na kuleta maendeleo ya soka

Mwakalebela  aliyewahi kuwa Katibu Mkuu wa (TFF),  amesema  akiingia madarakani atahakikisha kamati zitakazoteuliwa zitakuwa huru,atahakikisha zinafanya vikao vyake na kuzingatia kanuni, sheria na taratibu zilizowekwa, kuzingatia misingi ya utawala bora na kuhakikisha programu za maendeleo za timu za taifa za wanawake, wanaume, vijana na ufukweni zinafanyika ili kumaliza tatizo la kutofanya vizuri katika mashindano .
Pia amesema suala la mechi za Ligi Kuu Tanzania Bara kuwa na viporo halitakuwapo vile vile ataimarisha uhusiano na wadau wa mchezo huo hasa serikali.
Naye Mayai  anayewania nafasi hiyo iliyoachwa wazi na Jamal Malinzi amewaomba wajumbe kuchagua ili aweze kuleta mabadiliko ya uendeshaji wa soka .
Amesema akipata nafasi hiyo atashirikiana na wajumbe kukuza kiwango cha soka  na kutoa mfano wanawake wamekuwa wakifanya vizuri kwa sababu ya kushiriki katika mashindano mbalimbali.
 Mayai aliyeandamana na wachezaji wa zamani akiwamo Zamoyoni Mogella, Khalid Mohamed, Lawrence Mwalusako na Aaron Nyanda ametaja  vipaumbele vyake vingine ni kusimamia mpira wa miguu vizuri kuanzia ngazi ya vijana, wanawake na ngazi ya juu kwa weledi.

Naye Katibu Mkuu wa Mbeya City Emmanuel Kimbe, ambaye naye anawania nafasi hiyo ya juu amesema atahakikisha mchezo wa soka unarejesha heshima yake  kama ilivyokuwa miaka ya nyuma huku akiahidi kupambana kuboresha miundo mbinu ambayo sasa iko katika hali moja.


Mgombea Urais wa TFF,  Imani Madega akizungumza na waandishi wa habari leo wakati akizindua rasmi kampeni  yake  ya Uchaguzi wa unaotarajiwa kufanyika Jumamosi hii, Dodoma.

Imani Madega, Mwenyekiti wa zamani wa Yanga, amesema kuwa anaamini ana uwezo wa kuiongoza TFF kwa kuheshimu sheria na kusimamia uadilifu kama alivyofanya akiwa anaiongoza Yanga na kuacha kiasi cha Sh. milioni 200 wakati anaondoka madarakani.
Uchaguzi wa TFF unatarajiwa kufanyika keshokutwa mjini Dodoma na tayari wajumbe na wagombea wameshafika mkoani humo kuendelea kujinadi kwa wapiga kura.

Comments

Popular posts from this blog

Wachezaji waliosajiliwa na kuhama timu zote Ligi Kuu England

WAKATI dirisha la usajili Ulaya 2017 lililoanza Juni 9 lNdaniafungwa leo saa sita usiku, ifuatayo ni orodha ya wachezaji walioingia na kutoka katika timu 20 za Ligi Kuu England . Kama wewe ni shabiki wa moja ya timu hizo angalia orodha hii ujue wachezaji walioingia au kuondoka. ARSENAL Ndani Alexandre Lacazette - Lyon (ada haijatajwa), Sead Kolasac - Schalke(bure). Nje Wojciech Szczesny - Juventus, pauni 14m, Gabriel Paulista - Valencia, pauni 10m, Kieran Gibbs - West Brom, pauni 7m, Yaya Sanogo - ameachwa, Stefan O'Connor - ameachwa, Kristopher da Graca - ameachwa,Kostas Pileas - ameachwa, Takuma Asano - Stuttgart- mkopo Chris Willock - Benfica, (ada haijatajwa), Glen Kamara - ameachwa, Marc Bola - Bristol Rovers- mkopo Carl Jenkson - Birmgham- mkopo Cohen Bramall - Birmgham- mkopo Emiliano Martiez - Getafe-mkopo, Stephy Mavididi - Preston-mkopo, Ismael Bennacer - Empoli, (ada haijatajwa), Jon Toral - Hull, (ada haijatajwa). BOURNEMOUTH Ndani Asmir Begovic - Ch...

Zidane ajuta kumtwanga kichwa Materazzi

Picha mbili tofauti zinazomwonesha  Zinedine Zidane alipofanya tukio la kumpiga kichwa Marco Materazzi . MADRID, Hispania KOCHA wa timu ya  Real Madrid Zinedine Zidane amekumbuka tukio alilofanya kwa kumpiga kichwa aliyekuwa mlinzi wa timu ya taifa ya Italia,  Marco Materazzi katika kipindi chake cha mwisho cha uchezaji akisema kuwa hajisikii kujivuna kutokana na tukio hilo. Zidane alifanya tukio hilo wakati akiichezea Real Madrid, wakati akiitumikia Ufaransa katika mechi ya fainali ya kombe la Dunia 2006 ambayo iliisha kwa matokeo ya sare ya bao 1-1 kabla ya Azzuri kushinda kwa mikwaju ya penalti . Zidane ambaye alifanya mahojiano na kituo cha televisheni cha Ufaransa katika kipindi cha Telefoot na kuoneshwa kwenye runinga, alisema anajutia tukio hilo alilofanya katika siku za mwisho kama mchezaji. "Sijisikii kujivunia," Zidane alisema.  Zinedine Zidane akioneshwa kadi nyekundu kutokana na kumpiga kichwa  Marco Materazzi. "Sijivunii tuk...

Wazazi 'wamsusa' mpenzi wa Ronaldo mjamzito

Cristiano Ronaldo akiwa na Georgina Rodriguez na mtoto wao Ronaldo Jr MADRID, Hispania MPENZI wa Cristiano Ronaldo, Georgina Rodriguez anadaiwa kutengwa na wazazi wake. Mrembo huyo mwenye  umri wa miaka 23 anatarajia kujifungua mtoto wa kike Oktoba mwaka huu na kuongeza familia familia yake na Ronaldo inayokuwa kwa  haraka,  lakini kuna taarifa mama na baba yake hawajihusishi katika ujauzito huo. Kwa mujibu wa gazeti la Marca la Hispania, Rodriguez hamekuwan hana uhusiano mzuri na wazazi wake. Limeripoti kuwa kutokana na baba yeke Jorge Eduardo Rodriguez kuishi Argentina, na mama yake, Ana Maria Hernandez yuko nchini Italia, anamaliza kipindi chake cha ujauzito bila ya kupata sapoti. Mwanamitindo huyo mwenye damu mchanganyiko ya Kihispania na ki-Argentina mzaliwa wa Jaca kaskazini mashariki mwa Hispania, amebakia  katika nchi aliyozaliwa na sasa yuko na nyota wa Real Madrid ,anarajia kupata mtoto ambaye atakuwa wa nne kwa Ronaldo. Mtoto atakayemza...