![]() |
| Falcao akifunga bao pekee la ushindi |
PARIS, Ufaransa
MABINGWA watetezi wa Ligi Kuu Ufaransa, Monaco wameweka rekodi ya kushinda mechi 15 mfululizo katika ligi hiyo baada ya Radamel Falcao kufunga bao pekee dhidi ya Metz kwenye mchezo ambao Kylian Mbappe hakucheza.
Mbappe mwenye umri wa miaka18, aliachwa kwenye kikosi kitu ambacho kilizusha habari ziliunganisha tukio hilo na kuhamia katika timu ya Paris St-Germain.
Falcao alifunga bao hilo pekee dakika ya 78 baada ya kupata pasi kutoka kwa Rachid Ghezzal.
Baada ya kushinda mechi 12 katika msimu uliopita, Monaco imeanza ligi msimu huu kwa kuifunga Toulouse, Dijon na sasa Metz.
Ushindi iliopata Monaco umeifanya iivuke rekodi ya Bordeaux iliyokuwa imeshinda michezo 14 mfululizo 2009.
Mbappe, ambaye amekuwa akihusishwa na kuhamia Real Madrid na Manchester City, aliachwa kwenye kikosi na kocha ambaye amedai kumlinda mchezaji huyo.
Mshambuliaji huyo aling'ara katika msimu uliopita, alifunga mabao 26 katika mechi za mashindano yote, aliisaidia kutwaa ubingwa kwa mara ya kwanza baada ya kupita miaka 17 na kufika robo fainali.

Comments
Post a Comment