![]() |
| Haruna Niyonzima (kulia) baada ya kuwasili Dar es Salaam jana. |
KUWASILI kwa kinara upachikaji mabao katika Ligi Kuu ya Ghana, Nicholas Gyan na aliyekuwa mchezaji wa Yanga kwa misimu sita mfululizo na nahodha wa Rwanda, Haruna Niyonzima kumenogesha usajili wa kikosi cha Simba kwa msimu wa 2017- 2018.
Wawili hao ni wachezani wa mwisho wa kigeni kuwasili kabla ya kufungwa kwa dirisha la usajili usiku wa kuamkia leo.
Nyota hao walitua jana Uwanja wa Ndege wa Julius Nyerere (JNIA) mjini Dar es Salaam na kulakiwa na Kaimu Makamu Mwenyekiti wa Simba, Iddi Kajuna na viongozi wengine wa klabu, akiwemo Juma Ndambile .
Nicholas Gyan (kushoto) baada ya kuwasili Dar es Salaam , jana.
Wachezaji hao wa kigeni wanaungana na nyota wengine watano na kukamilisha idadi ya wachezaji saba wa kigeni, Method Mwanjali kutoka Zimbabwe ambaye alijiunga na wanamsimbazi hao msimu uliopita huku akiteuliwa kuwa nhodha katika msimu huu, Juuko Murshid na Emmanuel Okwi wote kutoka Uganda.
Wengine ni James Kotei (Ghana) na Laudit Mavugo kutoka Burundi. Nyota waliokuwa na timu hiyo msimu ulipita na kuachwa kwa kumaliza mikataba ni mlinda mlango Daniel Agyei (Ghana) na mshambuliaji Coast, Frederick Blagnon (Ivory Coast).
Haruna, Gyan na wachezaji wengine wanatarajiwa kutambulishwa rasmi kesho Agosti 8, 2017 katika siku ya Tamasha la Simba (Simba Day) linalofanyika kila mwaka katika tarehe hiyo, hutumika pia kutambulisha jezi na kuwakutanisha mashabiki wa Simba Pamoja kabla ya kauza kwa msimu.
Wachezaji wengine wapya waliosainiwa na timu hiyo ni, John Bocco, Shomary Kapombe, Erasto Nyoni, Aishi Manula (wote kutoka Azam), Said Mohamed, Salim Mbonde, Ally Shomary (wote Mtibwa), Emmanuel Mseja, Jamal Mwambeleko (wote Mbao FC), Paul Bukaba ( Atletico Olympic (burundi), Yusuph Mlipili (Toto African).
Siku hiyo ambayo ni hitimisho la Wiki ya Tamasha la Simba Day mbalia ya burudani kitahitimishwa na mchezo wa kirafiki dhidi ya mabingwa wa Rwanda, Rayon Sport Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.


Comments
Post a Comment