Skip to main content

McGregor kumpiku Ronaldo kimapato

Conor McGregor (kushoto) alipokutana na Cristiano Ronaldo. 
NEW YORK, Marekani
BONDIA Conor McGregor anajiandaa kumpiku Cristiano Ronaldo kwa kupata mapato mengi katika orodha ya Jarida la Forbes linaloandika  kuhusu mapato na utajiri wa wanamichezo na watu maarufu baada ya pambano lake dhidi ya Floyd Mayweather lililofanyika Jumapili iliyopita.
Mpiganaji huyo mzaliwa wa Dublin, Scotland anatarajiwa kuingia fedha kiasi cha pauni milioni 77 (zaidi ya sh. bilioni 223) bila ya kujumuisha matangazo ya biashara.
Ronaldo aliongoza kwa kupata mapato mengi mwaka huu aliingiza pauni milioni 71(zaidi ya sh. bilioni 205), anaweza kuzidiwa mapato baada ya McGregor kutwangana na Mayweather kwa raundi 10 mjini Las Vegas na kupigwa kwa TKO, mwamuzi alisimamisha pambano baada ya kuona anazidiwa.
Ronaldo anachezea timu ya Real Madrid na McGregor walikutana mwaka jana na kuzungumza na kutaniana kwa kupigana. 
Ronaldo ndiye alimtembelea kambini McGregor ambaye ni bingwa wa ngumi mchanganyiko (UFC) uzani wa light na bondia huyo alimtania kwa kumwambia: Umekuwa namba moja katika orodha ya Forbes, ninapenda kuwa wa 35 au namba nyingine. Nitapanda. Pengine mwaka ujao nitakukuta.' Ronaldo alijibu: 'Sifikiri hivyo.'
McGregor hatakuwa namba moja kwenye orodha ya Forbes ijayo,Mayweather anaweza kuongoza. 
Baadhi ya taarifa zinasema  Mayweather 'Money' anatarajiwa kupata pauni milioni 233 (zaidi ya sh. bilioni 674.5) kutokana na mapato ya pambano lake la mwishoni mwa wiki mjini Las Vegas. 
Lakini mabondia hao wanatarajiwa kuwapita kimapato wananamichezo kama LeBron James, Roger Federer na Lewis Hamilton. 
Forbes katika kufanya mchanganuo wa mapato  hujumuisha mishahara na bonasi zinazopatikana katika mwaka.

Comments

Popular posts from this blog

Wachezaji waliosajiliwa na kuhama timu zote Ligi Kuu England

WAKATI dirisha la usajili Ulaya 2017 lililoanza Juni 9 lNdaniafungwa leo saa sita usiku, ifuatayo ni orodha ya wachezaji walioingia na kutoka katika timu 20 za Ligi Kuu England . Kama wewe ni shabiki wa moja ya timu hizo angalia orodha hii ujue wachezaji walioingia au kuondoka. ARSENAL Ndani Alexandre Lacazette - Lyon (ada haijatajwa), Sead Kolasac - Schalke(bure). Nje Wojciech Szczesny - Juventus, pauni 14m, Gabriel Paulista - Valencia, pauni 10m, Kieran Gibbs - West Brom, pauni 7m, Yaya Sanogo - ameachwa, Stefan O'Connor - ameachwa, Kristopher da Graca - ameachwa,Kostas Pileas - ameachwa, Takuma Asano - Stuttgart- mkopo Chris Willock - Benfica, (ada haijatajwa), Glen Kamara - ameachwa, Marc Bola - Bristol Rovers- mkopo Carl Jenkson - Birmgham- mkopo Cohen Bramall - Birmgham- mkopo Emiliano Martiez - Getafe-mkopo, Stephy Mavididi - Preston-mkopo, Ismael Bennacer - Empoli, (ada haijatajwa), Jon Toral - Hull, (ada haijatajwa). BOURNEMOUTH Ndani Asmir Begovic - Ch...

Zidane ajuta kumtwanga kichwa Materazzi

Picha mbili tofauti zinazomwonesha  Zinedine Zidane alipofanya tukio la kumpiga kichwa Marco Materazzi . MADRID, Hispania KOCHA wa timu ya  Real Madrid Zinedine Zidane amekumbuka tukio alilofanya kwa kumpiga kichwa aliyekuwa mlinzi wa timu ya taifa ya Italia,  Marco Materazzi katika kipindi chake cha mwisho cha uchezaji akisema kuwa hajisikii kujivuna kutokana na tukio hilo. Zidane alifanya tukio hilo wakati akiichezea Real Madrid, wakati akiitumikia Ufaransa katika mechi ya fainali ya kombe la Dunia 2006 ambayo iliisha kwa matokeo ya sare ya bao 1-1 kabla ya Azzuri kushinda kwa mikwaju ya penalti . Zidane ambaye alifanya mahojiano na kituo cha televisheni cha Ufaransa katika kipindi cha Telefoot na kuoneshwa kwenye runinga, alisema anajutia tukio hilo alilofanya katika siku za mwisho kama mchezaji. "Sijisikii kujivunia," Zidane alisema.  Zinedine Zidane akioneshwa kadi nyekundu kutokana na kumpiga kichwa  Marco Materazzi. "Sijivunii tuk...

Wazazi 'wamsusa' mpenzi wa Ronaldo mjamzito

Cristiano Ronaldo akiwa na Georgina Rodriguez na mtoto wao Ronaldo Jr MADRID, Hispania MPENZI wa Cristiano Ronaldo, Georgina Rodriguez anadaiwa kutengwa na wazazi wake. Mrembo huyo mwenye  umri wa miaka 23 anatarajia kujifungua mtoto wa kike Oktoba mwaka huu na kuongeza familia familia yake na Ronaldo inayokuwa kwa  haraka,  lakini kuna taarifa mama na baba yake hawajihusishi katika ujauzito huo. Kwa mujibu wa gazeti la Marca la Hispania, Rodriguez hamekuwan hana uhusiano mzuri na wazazi wake. Limeripoti kuwa kutokana na baba yeke Jorge Eduardo Rodriguez kuishi Argentina, na mama yake, Ana Maria Hernandez yuko nchini Italia, anamaliza kipindi chake cha ujauzito bila ya kupata sapoti. Mwanamitindo huyo mwenye damu mchanganyiko ya Kihispania na ki-Argentina mzaliwa wa Jaca kaskazini mashariki mwa Hispania, amebakia  katika nchi aliyozaliwa na sasa yuko na nyota wa Real Madrid ,anarajia kupata mtoto ambaye atakuwa wa nne kwa Ronaldo. Mtoto atakayemza...