![]() |
| Floyd Mayweather (kushoto( na Conor McGregor walipokutana uso kwa uso Marekani |
LAS VEGAS, Marekani
MABONDIA Floyd Mayweather na bingwa wa UFC light uzani Conor McGregor wamefanya mkutano mbele ya waandishi wa habari kabla ya pambano lao la jumamosi na kila mmoja amemtambia mwenzie kuwa atamtwanga.
Lakini katika Tambio hizo cha ajabu Conor McGregor amesema kama ingeruhusisha atumie sanaa mapigano mchanganyiko (ngumi, mieleka, mateke) ambayo amekuwa akipigana mda mrefu angemtwanga kwa haraka zaidi mpinzani wake.
Walifanya mkutano wao jana katika Ukumbi wa MGM Grand mjini Las Vegas huku na walionekana kuwa wastaarabu kidogo lakini vijembe havikukosekana.
Pambano lao litakalofanyika uwanja wa T-Mobile Arena linatajwa litakuwa la malipo makubwa zaidi katika historia ya ngumi, McGregor (29) anatarajiwa kupata dola milioni 100, imeleta uvumi kuwa huenda baada ya pambano hilo linaweza asiendelea kupigana katika taasisi aliyokuwa akipigania.
Pambano hilo litaoneshwa kwa njia ya televisheni katika nchi zaidi ya 220.
![]() |
| Floyd Mayweather (wapili kushoto( r na Conor McGregor wakiwa mbele ya waandishi wa habari ambao hawapo pichani. |
McGregor alisema katika pambano hilo anaweza kutumia sekunde 20 na kupata ushindi kisha kufikiria ni bondia gani mwingine atapigana naye.
Mayweather katika mkutano huo hakuonekana hakuonekana kutaka kutukanana na mpinzani wake, kitu ambacho kimetajwa pengine ni kutokana na kapuni za kubeti kuweka kipengele hicho.
Alisema anataka kushinda pambano hilo ili kuwa na rekodi ya kushinda mapambano 50 katika mechi 50 bila ya kupigwa.
"McGregor anaweza kusema anachotaka, pambano likija nitapigana. " Kiakiri, hakuna mwanamichezo aliye imara kama mimi. Nimekuwa katika mchezo huu nikifanya vizuri kwa miaka 21. Nyie mnafikiri kuwa silichukulii pambano hilo kwa uzito? ninalipa uzito,'' alisema
Imeelezwa kuwa mshindi wa pambano hilo atapatiwa mkanda Kutoka Barala za Ngumi la Dunia (WBC) umepewa jina la 'The Money Belt'.


Comments
Post a Comment