![]() |
| Floyd Mayweather (kushoto) alipokuwa akitambiana Conor McGregor. |
NEW YORK, Marekani
BONDIA Floyd Mayweather amesema Conor McGregor ana nafasi kubwa ya kushinda pambano lao linalotarajiwa kufanyika mwezi huu.
Mayweather ambaye hajapoteza pambano katika mapigano 49 aliyocheza, atatwangana na mpiganaji nyota wa ngumi mchanganyiko zinazohusisha mateke, mieleka McGregory katika Ukumbi wa T-Mobile Arena mjini Las Vegas, Marekani, pambano linalotajwa kuwa la fedha nyingi zaidi katika historia.
Wawili hao walitukanana na kutoleana vitisho katika miji minne waliyokwenda kutangaza pambano lao, huku karibuni Mayweathe akisema atamtwanga kwa KO, McGregor.
Akizungumza na ESPN, Mayweather alisema McGregor ni kijana na ni mrefu zaidi ni mkubwa kuanzia chini hadi juu.
'' Yeye ni kijana sana. Ujana uko upande wake. Nimekuwa nje ya ulingo kwa miaka. Mimi niko katika miaka 40. Kama ukiangalia katika kila gazeti inaonesha Conor McGregor anapewa nafasi,'' alisema.
''Mimi ni mzee, sina kiwango kama nilichokuwa nacho miaka miwili iliyopita. Siko kama nilivyokuwa miaka mitano iliyopita. Nimepoteza hatua.
''Mpiganaji kama Andre Berto hakuwa wa kiwango cha kupigana na Floyd Mayweather, lakini kumbuka nilikuwa na umri wa miaka 38,'' alisema.
Hata hivyo, Mayweather anapewa nafasi ya kushinda pambano hilo baada ya kushinda mapambano yake yote 49. McGregor, hajawahi kupigana chini ya sheria za ngumi.
Mayweather ameadhidi siku ya pambano kucheza mchezo wa kufurahisha natatumi mbinu kama alizotumia katika pambano lake dhidi ya Manny Pacquiao.
Alisema: '' Mchezo huu hauwezi kuwa wa kujilinda. Nitakwenda mbele. Ninatajitolea kwa ajili ya mashabiki kwa sababu ya pambano la Pacquiao. Hawakufurahishwa na uchezaji wangu. Watafurahi safari hii.''

Comments
Post a Comment