Mwandishi wetu
WAKATI
kikosi cha Simba kinatarajiwa kurejea Dar es Salaam kutokea Afrika Kusini ilikoweka
kambi kwa ajili ya maandalizi ya msimu mpya kesho kutwa ,mashabiki wanajipanga
kufanya mapokezi makubwa ya kiungo wake mpya Haruna Niyonzima.
Niyonzima
ambaye ametangazwa rasmi juzi na Ofisa wa Habari wa Simba, Haji Manara kuwa
sasa ni mchezaji halali klabu hiyo, yuko
nchini kwao Rwanda baada ya kuomba
ruhusa kutatua matatizo yake binafsi, anatarajiwa kuungana na timu yake mpya
itakapotoka Afrika Kusini.
Habari
ilizonazo Spotifleva mashabiki wengi wa klabu hiyo wanapanga kufanya mapokea
makubwa ya Niyonzima ambaye amasjiunga na klabu yao akitokea Yanga
aliyoitumikia kwa mafanikio makubwa kwa misimu sita.
“Tunajipanga
kufanya mapokezi makubwa kwa Niyonzima ambaye tunaamini kuwa kwa kushiriana na
wachezaji wenzie wataifanyia mambo makubwa timu yetu katika msimu huu,” alisema
mwanachama wa klabu hiyo aliyejitambulisha na kwa jina Juma Hussein.
Baada
ya kuwasili ataungana na wacheaji wenzie wa Simba ambao watafanya shughuli
mbalimbali za kijamii katika wiki ya samba iliyozinduliwa rasmi juzi.
Niyonzima
ananatarajiwa kutambulishwa rasmi katika Siku ya Simba Agosti 8 mwaka huu kwenye uwanja wa Taifa Dar es Salaam sanjari
na wacheaji wengine wote wa Simba ambapo kutakuwa na mchezo dhidi ya Rayon
Sports ya Rwanda, pamoja na siku hiyo kupambwa kwa burudani pia jezi mpya
zitakaotumia na klabu hiyo zitaoneshwa kwa mashabiki.
Baada
ya mchezo wake na Rayon, Simba aitaingia tena kambini kujianda wka mchezo wake
wa Ngao ya Jamii dhidi ya Yanga ukakaofanyika Agosti 23, kwenye Uwanja wa taifa
Dar es Salaam kabla ya kuanza Ligi Kuu ya Vodacom Agosti 26, mwaka huu.

Comments
Post a Comment