![]() |
| Cristiano Ronaldo akishangilia baada ya kuifungia Real Madrid bao la pili dhidi ya Barcelona. |
TIMU ya Real Madrid imetwaa kombe la Supercopa la Hispania kwa kuwafunga mahasimu wao Barcelona mabao 3-1.
Katika mchezo huo uliopigwa uwanja wa Camp Nou usiku wa kuamkia leo , mshambuliaji Cristiano Ronaldo aliingia akitokea benchi na kufunga bao la pili kabla ya kutolewa kwa kuoneshwa kadi ya njano ya pili muda mfupi baadaye.
Alipofunga bao wakati wa kushangilia alivua jezi na kubakia kufua wazi, akiwaonesha mashabiki jezi yake yenye namba 7, refa alimwonesha kadi ya njano ya kwanza kwa kitendo hicho, kadi ya pili alioneshwa kwa kile mwamuzi alichoona kama ni kudanganya kujiangusha katika eneo la penalti la timu pinzani.
Wakati akitoka uwanjani alimsukuma refa kwa kukasirishwa na kadi aliyompatia.
![]() |
| Lionel Messi akitoka uwqanjani kichwa chini baada ya timu ya kufungwa mabao 3-1. |
Madrid inayonolewa na Zinedine Zidane, ilipata bao la kwanza mwanzoni mwa kipindi ya pili lililotokana na Gerard Pique kujifunga lakini Barca ilisawazisha kwa penalti iliyopigwa na Lionel Messi baada ya ya kuonekana kama Luis Suarez alichezewa faulo.
Bao la tatu la Madrid lilifungwa na Marco Asensio.
Timu hizo zitarudiana tena Jumatano katika Uwanja wa Santiago Bernabeu ikiwa ni mara ya kwanza zinakutana kuwania taji hilo tangu mwaka 2012.
Taji la Supercopa huwani na timu iliyotwaa ubingwa wa Laliga (Madrid) na ile iliyotwaa Copa de la Ray (Barcelona).


Comments
Post a Comment