LONDON, Uingereza
TIMU za Real Madrid na Manchester United zitaifanya Dunia kusimama kwa muda leo, wakati zitakapokuwa zikipambana katika mchezo wa kuwania Kombe la Shirikisho la Mpira wa Miguu Ulaya (Uefa Super Cup).
Kama United itafanikiwa kushinda mchezo huo utakaoanza saa 3:15 mjini Skopje, Macedonia, itakuwa imetwaa taji la nne kwa mwaka huu.
Super Cup huwaniwa na timu iliyotwaa taji la Ligi ya Mabingwa kwa msimu uliotangulia (Real Madrid) na bingwa wa Ligi ya Europa ( Man United).
United ikiwa chini ya Jose Mourinho ilianza msimu uliopita Agosti, mwaka jana kwa kuifunga Leicester na kutwaa Ngao ya Jamii, kisha ikaifunga Southampton katika fainali ya Kombe la EFL Cup na kuichapa Ajax katika fainali ya Ligi ya Europa.
Kama United itaifunga Real itakuwa ni mara yake ya nne katika historia yake kutwaa makombe manne katika mwaka mmoja.
Mashetani Wekundu hao walishinda mara mbili dhidi ya timu za Hispania kati ya mara 10, ikishinda mara moja kati ya mechi tano zilizochezwa ugenini na nyumbani.
Manchester United ikishinda inaweza kutwaa taji lake la pili la Super Cup baada ya mara ya mwisho kulitwaa 1991 walipoifunga Red Star Belgrade bao 1-0 katika Uwanja wa Old Trafford.
United Inaweza kuwa timu ya pili ya Uingereza kutwaa mara mbili Super Cup, nyuma ya Liverpool iliyotwaa kombe hilo mara tatu.
Kocha Jose Mourinho amepoteza mara mbili katika kuwania taji hilo akiwa kocha, 2013 alipokuwa na Chelsea mwaka 2003 alipokuwa na FC Porto.
Mourinho anakuwa kocha wa kwanza kuzinoa timu tatu tofauti katika kuwania taji hilo.
Timu za Hispania zimetwaa taji hilo mara saba kati ya nane, timu ya mwisho ikiwa ni Atletico Madrid (2012) walipoifunga Chelsea mabao 4-1, ni timu ya Barcelona na AC Milan pekee zimewahi kutwaa taji hilo mara tano huku Real ikilitwaa mara tatu.
Cristiano Ronaldo ambaye leo atakuwemo kwenye kikosi cha Madrid ameweka rekodi ya kufunga jumla ya mabao 108 katika mashindano yote ya Ulaya ikiwemo mawili katika Super Cup.
United, katika mchezo wa leo itamkosa Eric Bailly na Phil Jones ambao anatumikia adhabu kitu ambacho kitatoa nafasi kwa mchezaji mpya Victor Lindelof kucheza.
Wachezaji wengine wapya wa United ni wanaoweza kucheza leo ni Romelu Lukaku na kiungo Nemanja Matic.
Real imewaongeza mchezaji kijana Theo Hernandez na Dani Ceballos katika kikosi chake ambacho msimu uliopita kilitwaa ubingwa wa Liga Liga na Ligi ya Mabingwa msimu uliopita, wanaweza kuunga na Sergio Ramos katika sehemu ya ulinzi.
United katika mechi za kujiandaa na msimu iliifunga Real kwa penalti baada ya kutoka sare ya bao 1-1 katika mchezo wa kirafiki uliopigwa California mwezi uliopita na kushinda mechi tano za maandalizi ya msimu, ikipoteza mchezo mmoja tu kwa Barcelona.
Real, kwa upande wake ilishindwa kushinda mchezo wowote kati ya minne ya kirafiki nchini Marekani katika dakika 90 minutes, ikipoteza kwa mabao 3-2 dhidi ya Barca na kufungwa mabao 4-1 dhidi ya Manchester City, ushindi wake pekee ulikuwa dhidi ya timu ya MLS All.
Timu zinazotarajiwa kuanza ni
Je, ni timu gani itaibuka na ushindi katika mchezo wa leo utakaoanza saa 3:45? Dakika 90 za mchezo zitaamua.


Comments
Post a Comment