Skip to main content

Liverpool yafanya kweli kumsaini Keita


Naby Keita 

LONDON, Uingereza
KLABU ya Livepool msimu huu imeamua kufanya kweli kwa kusaini wachezaji anaoamini wanaweza kuisaidia timu yao kuwa vizuri na kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu ya England ambao hawajautwaa kwa za zadi ya miaka 20 na kutaka kufanya vizuri katika mashindano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya.
Liverpool  inayonolewa na kocha Mjerumani, Jurgen Klopp imekubali kulipa ada ya pauni milioni 60 (zaidi ya Sh. bilioni 174) ambayo itavunja rekodi yake ya usajili kwa kumsaini mchezaji wa  Kiafrika, Naby Keita kutoka timu ya RB Leipzig ya Ujerumani.
Nyota huyo raia wa Ghana jana alifanyiwa vipimo England, lakini atabakia na timu ya Leipzig msimu huu kabla ya kujiunga na Liverpool msimu ujao chanzo kimesema.
Liverpool ilikuwa ikimfuatilia nyota huyo anayecheza katika sehemu ya kiungo msimu huu, awali ilituma ofa mbili ambazo zilikataliwa na Leipzig  iliyoshika nafasi ya pili katika Bundesliga, ofa ya pili ilikuwa na thamani ya pauni milioni 69.3, alisema mmiliki mwenza wa, Red Bull, Dietrich Mateschitz.
Leipzig ilikuwa ikisema wazi kwamba Keita hauzwi kwa bei yoyote katika majira haya ya joto kwa kuwa klabu inataka kumtumia katika ligi ya ndani na Ligi ya Mabingwa ambayo wanashiriki kwa mara ya kwanza katika historia yao.
Hata hivyo, mkataba wa Keita una kipengele cha kuuvunja kwa pauni milioni 48 kuanzia Julai Mosi 2018,  Liverpool imekubali kulipa fedha hizo pamoja na kiasi kingine ambacho hakijawekwa wazi lakini inadaiwa jumla yake kufikia pauni milioni 60.
Kwa kumsaini mcheaji huyo ina maana imevunja rekodi ya wachezaji wake wengine iliowasaini kwa fedha nyingi, wa mwisho akiwa ni Andy Carroll  iliyomsaini kwa pauni milioni  35 (zaidi ya sh. bilioni 10) mwaka  2011 akitokea Newcastle.
Liverpool jana ilithibitisha kuwa imalizana na RB Leipzig na Keita alisema: "Kilichomfuarahisha ni sana ni kuwa sehemu ya  mradi wa Liverpool wa kuofanya klabu kuwa imara zaidi.''
Alisema kwa sasa ataendelea kuweka mtazamo na  kuwajibika kwa timu yake kwa muda uliosalia ili kufanikisha malengo ya msimu huu, huku akijua ana hatima yake ya baadaye.
Katika majira haya ya joto, Liverpool imewasaini winga Mohamed Salah kutoka Roma kwa pauni milioni 34 (zaidi ya sh bilioni 98.6), mlinzi Andrew Robertson kutoka Hull kwa ada ya pauni milioni 8 (zaidi ya sh. bilioni 23 na mshambuliaji Dominic Solanke kama mchezaji huru akitokea Chelsea alikomaliza mkataba wake.
Miamba hiyo ya Anfield kwa sasa pia inajipanga  kumsaini kiungo wa Monaco, Thomas Lemar kwa ada ya pauni milioni 60 ( zaidi ya sh. bilioni 174  kabla ya dirisha la usajili kufungwa Alhamisi hii.

Comments

Popular posts from this blog

Wachezaji waliosajiliwa na kuhama timu zote Ligi Kuu England

WAKATI dirisha la usajili Ulaya 2017 lililoanza Juni 9 lNdaniafungwa leo saa sita usiku, ifuatayo ni orodha ya wachezaji walioingia na kutoka katika timu 20 za Ligi Kuu England . Kama wewe ni shabiki wa moja ya timu hizo angalia orodha hii ujue wachezaji walioingia au kuondoka. ARSENAL Ndani Alexandre Lacazette - Lyon (ada haijatajwa), Sead Kolasac - Schalke(bure). Nje Wojciech Szczesny - Juventus, pauni 14m, Gabriel Paulista - Valencia, pauni 10m, Kieran Gibbs - West Brom, pauni 7m, Yaya Sanogo - ameachwa, Stefan O'Connor - ameachwa, Kristopher da Graca - ameachwa,Kostas Pileas - ameachwa, Takuma Asano - Stuttgart- mkopo Chris Willock - Benfica, (ada haijatajwa), Glen Kamara - ameachwa, Marc Bola - Bristol Rovers- mkopo Carl Jenkson - Birmgham- mkopo Cohen Bramall - Birmgham- mkopo Emiliano Martiez - Getafe-mkopo, Stephy Mavididi - Preston-mkopo, Ismael Bennacer - Empoli, (ada haijatajwa), Jon Toral - Hull, (ada haijatajwa). BOURNEMOUTH Ndani Asmir Begovic - Ch...

Zidane ajuta kumtwanga kichwa Materazzi

Picha mbili tofauti zinazomwonesha  Zinedine Zidane alipofanya tukio la kumpiga kichwa Marco Materazzi . MADRID, Hispania KOCHA wa timu ya  Real Madrid Zinedine Zidane amekumbuka tukio alilofanya kwa kumpiga kichwa aliyekuwa mlinzi wa timu ya taifa ya Italia,  Marco Materazzi katika kipindi chake cha mwisho cha uchezaji akisema kuwa hajisikii kujivuna kutokana na tukio hilo. Zidane alifanya tukio hilo wakati akiichezea Real Madrid, wakati akiitumikia Ufaransa katika mechi ya fainali ya kombe la Dunia 2006 ambayo iliisha kwa matokeo ya sare ya bao 1-1 kabla ya Azzuri kushinda kwa mikwaju ya penalti . Zidane ambaye alifanya mahojiano na kituo cha televisheni cha Ufaransa katika kipindi cha Telefoot na kuoneshwa kwenye runinga, alisema anajutia tukio hilo alilofanya katika siku za mwisho kama mchezaji. "Sijisikii kujivunia," Zidane alisema.  Zinedine Zidane akioneshwa kadi nyekundu kutokana na kumpiga kichwa  Marco Materazzi. "Sijivunii tuk...

Wazazi 'wamsusa' mpenzi wa Ronaldo mjamzito

Cristiano Ronaldo akiwa na Georgina Rodriguez na mtoto wao Ronaldo Jr MADRID, Hispania MPENZI wa Cristiano Ronaldo, Georgina Rodriguez anadaiwa kutengwa na wazazi wake. Mrembo huyo mwenye  umri wa miaka 23 anatarajia kujifungua mtoto wa kike Oktoba mwaka huu na kuongeza familia familia yake na Ronaldo inayokuwa kwa  haraka,  lakini kuna taarifa mama na baba yake hawajihusishi katika ujauzito huo. Kwa mujibu wa gazeti la Marca la Hispania, Rodriguez hamekuwan hana uhusiano mzuri na wazazi wake. Limeripoti kuwa kutokana na baba yeke Jorge Eduardo Rodriguez kuishi Argentina, na mama yake, Ana Maria Hernandez yuko nchini Italia, anamaliza kipindi chake cha ujauzito bila ya kupata sapoti. Mwanamitindo huyo mwenye damu mchanganyiko ya Kihispania na ki-Argentina mzaliwa wa Jaca kaskazini mashariki mwa Hispania, amebakia  katika nchi aliyozaliwa na sasa yuko na nyota wa Real Madrid ,anarajia kupata mtoto ambaye atakuwa wa nne kwa Ronaldo. Mtoto atakayemza...