![]() |
| Kikosi cha timu ya Lipuli FC ya Iringa ambayo imepanda daraja msimu huu. |
LIGI Kuu ya msimu ujao itakuwa na timu 20 badala ya 16 za sasa kitu kitakachofanya timu kucheza mechi nyingi zaidi na ligi Kuchukua nmuda mrefu.
Uamuzi wa kuongeza idadi ya timu umefanywa na Kamati ya Utendaji ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) iliyokutana Jumanne Agosti 22, 2017 na ku fanya marekebisho ya Kanuni za Ligi Daraja la Kwanza inayotarajiwa kuanza Septemba 16, mwaka huu.
Kwa kuwa na timu 20 ina maana Ligi Kuu ya Tanzania itakuwa na idadi ya timu kama ilivyo Ligi Kuu ya England, Hispania, Italia, Ufaransa na ligi nyingine kubwa.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa jana na TFF kupiti kwa katibu Mkuu wake, Alfred Lucas timu zitakazoshuka Ligi Kuu ya Vodacom baada ya kuisha msimu huu zitakuwa mbili na kubaki 14.
Ili kufikia timu 20, zitapanfa timu sita (6) za Ligi Daraja la Kwanza.
Tayari TFF imetangaza makundi matatu yenye timu nane kila moja katika Ligi ya Daraja la Kwanza msimu huu itakayoanza Septemba 16, mwaka huu, ikiwa na maana kila kundi zitapanda timu mbili.
Kundi ‘A’ lina timu za African Lyon, Ashanti United, Friends Rangers za Dar es Salaam, JKT Ruvu na Kiluvya United za Pwani, Mgambo JKT ya Tanga, Mvuvumwa ya Kigoma na Polisi Moro ya Morogoro.
Kundi ‘B’ ziko za Coastal Union ya Tanga; JKT Mlale ya Ruvuma; KMC ya Dar es Salam, Mawezi Market ya Morogoro, Mbeya Kwanza ya Mbeya, Mufundi United ya Iringa, Mshikamano na Polisi Dar za Dar es Salaam.
Kundi ‘C’ lina timu za Alliance School, Pamba na Toto African za Mwanza, Rhino Rangers ya Tabora, Polisi Mara ya Mara, Polisi Dodoma ya Dodoma, Transit Camp ya Shinyanga na JKT Oljoro ya Arusha.
Timu zilizoshuka Ligi Kuu msimu uliopita ni Toto African, Arivan Lyon na JKT Ruvu wakati zilizopanda ni Singida Unite, Mjini Njombe na Lipuli.

Comments
Post a Comment