Skip to main content

Klopp aitabiria ubingwa Manchester City



Jugern Klopp (kulia) akitaniana na Pep Guardiola katika moja ya mechi zilizokutanisha timu zao.


LONDON, Uingereza

JURGEN Klop amesema timu ya Manchester City ni ya kipekee anaipa nafasi kubwa kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu England msimu huu.

Kocha huyo wa Liverpool naye  amemshambulia Pep Guardiola kwa kutumia fedha nyingi kusajili.

Alisema hayo kabla ya Ligi Kuu England kuanza leo, Arsenal ikipambana na Leicester City, Kocha huyo wa zamani wa Borussia Dortmund amesema Pep, kwa kumsaini Gabriel Jesus na wachezaji wengine katika majira haya ya joto imefanya timu yake kuwa imara zaidi.

Wachezaji wengine waliosainiwa na City ni beki Benjamin Mendy, Kyle Walker na Danilo amewaondoa Bernardo Silva  na Ederson katika Uwanja wa Etihad walioiingizia timu zaidi ya pauni milioni 26.

Klopp aliiiambia DAZN: “ Timu inayopewa nafasi lazima itakuwa Manchester City. Walicheza soka ya kusisimua msimu uliopita na ilikuwa na matatizo machache. Wao wazi kabisa wana nafasi. Safu yao ya ushambuliaji  iliyoundwa na vijana ni nzuri,''

Klopp (50) ambaye timu yake itaanza kampeni ya ligi ugenini Vicarage Road dhidi ya Watford kesho alisema anatumaini msimu huu kumaliza juu kadiri iwezekanavyo.

Pia alisema anatumaini Manchester United itatoa ushindani mkubwa sanjali na Chelsea ambayo haitakwua na  Costa lakini imemsajili [Alvaro] Morata na kumpoteza [Nemanja] Matic.

Comments

Popular posts from this blog

Wachezaji waliosajiliwa na kuhama timu zote Ligi Kuu England

WAKATI dirisha la usajili Ulaya 2017 lililoanza Juni 9 lNdaniafungwa leo saa sita usiku, ifuatayo ni orodha ya wachezaji walioingia na kutoka katika timu 20 za Ligi Kuu England . Kama wewe ni shabiki wa moja ya timu hizo angalia orodha hii ujue wachezaji walioingia au kuondoka. ARSENAL Ndani Alexandre Lacazette - Lyon (ada haijatajwa), Sead Kolasac - Schalke(bure). Nje Wojciech Szczesny - Juventus, pauni 14m, Gabriel Paulista - Valencia, pauni 10m, Kieran Gibbs - West Brom, pauni 7m, Yaya Sanogo - ameachwa, Stefan O'Connor - ameachwa, Kristopher da Graca - ameachwa,Kostas Pileas - ameachwa, Takuma Asano - Stuttgart- mkopo Chris Willock - Benfica, (ada haijatajwa), Glen Kamara - ameachwa, Marc Bola - Bristol Rovers- mkopo Carl Jenkson - Birmgham- mkopo Cohen Bramall - Birmgham- mkopo Emiliano Martiez - Getafe-mkopo, Stephy Mavididi - Preston-mkopo, Ismael Bennacer - Empoli, (ada haijatajwa), Jon Toral - Hull, (ada haijatajwa). BOURNEMOUTH Ndani Asmir Begovic - Ch...

Zidane ajuta kumtwanga kichwa Materazzi

Picha mbili tofauti zinazomwonesha  Zinedine Zidane alipofanya tukio la kumpiga kichwa Marco Materazzi . MADRID, Hispania KOCHA wa timu ya  Real Madrid Zinedine Zidane amekumbuka tukio alilofanya kwa kumpiga kichwa aliyekuwa mlinzi wa timu ya taifa ya Italia,  Marco Materazzi katika kipindi chake cha mwisho cha uchezaji akisema kuwa hajisikii kujivuna kutokana na tukio hilo. Zidane alifanya tukio hilo wakati akiichezea Real Madrid, wakati akiitumikia Ufaransa katika mechi ya fainali ya kombe la Dunia 2006 ambayo iliisha kwa matokeo ya sare ya bao 1-1 kabla ya Azzuri kushinda kwa mikwaju ya penalti . Zidane ambaye alifanya mahojiano na kituo cha televisheni cha Ufaransa katika kipindi cha Telefoot na kuoneshwa kwenye runinga, alisema anajutia tukio hilo alilofanya katika siku za mwisho kama mchezaji. "Sijisikii kujivunia," Zidane alisema.  Zinedine Zidane akioneshwa kadi nyekundu kutokana na kumpiga kichwa  Marco Materazzi. "Sijivunii tuk...

Wazazi 'wamsusa' mpenzi wa Ronaldo mjamzito

Cristiano Ronaldo akiwa na Georgina Rodriguez na mtoto wao Ronaldo Jr MADRID, Hispania MPENZI wa Cristiano Ronaldo, Georgina Rodriguez anadaiwa kutengwa na wazazi wake. Mrembo huyo mwenye  umri wa miaka 23 anatarajia kujifungua mtoto wa kike Oktoba mwaka huu na kuongeza familia familia yake na Ronaldo inayokuwa kwa  haraka,  lakini kuna taarifa mama na baba yake hawajihusishi katika ujauzito huo. Kwa mujibu wa gazeti la Marca la Hispania, Rodriguez hamekuwan hana uhusiano mzuri na wazazi wake. Limeripoti kuwa kutokana na baba yeke Jorge Eduardo Rodriguez kuishi Argentina, na mama yake, Ana Maria Hernandez yuko nchini Italia, anamaliza kipindi chake cha ujauzito bila ya kupata sapoti. Mwanamitindo huyo mwenye damu mchanganyiko ya Kihispania na ki-Argentina mzaliwa wa Jaca kaskazini mashariki mwa Hispania, amebakia  katika nchi aliyozaliwa na sasa yuko na nyota wa Real Madrid ,anarajia kupata mtoto ambaye atakuwa wa nne kwa Ronaldo. Mtoto atakayemza...