LONDON, Uingereza
KOCHA wa Arsenal, Arsene Wenger amesema hakumbuki ni wakati gani timu hiyo aliyoinoa kwa zaidi ya miaka 20 imewahi kucheza vibaya kana iliyocheza na Liverpool na kupata kipata kipigo cha matendegu ya kitanda (mabao 4-0).
Amewataka mashabiki radhi na kuwaomba kuendelea kuwa pamoja na timu baada ya kipigo cha timu yao alichokiita kama ni janga na udhalilishaji
"Kama kuna watu wanahisi mimi ni tatizo, ninawataka radhi kwamba mimi ni tatizo," Wenger aliiambia Sky Sports.
"Lakini tunataka mashabiki wetu kuwa na sisi hata wakati tunapopoteza kama vile."
Alisema: " Kitu pekee ambacho tunaweza kufanya ni kurejea nyuma kujiandaa na kuja kucheza vizuri."
Katika mchezo huo, uliopigwa uwanja wa Anfield wachezaji wake walionekana kama walikuwa hataki kuwepo uwanjani na kocha kuonekana kama amemepotea njia hajui aende wapi.
Baadhi ya mashabiki wa Arsenal nao wamechanganyikiwa wanajiuliza ni kwanini kocha wao alimwacha katika benchi mchezaji ghari kwenye timu hiyo aliyemsaini msimu huu Alexandre Lacazette ( kwa pauni milioni 53 ambazo nji zaidi ya ya sh. bilioni 152.7)
Kwa kipigo hicho, Arsenal haijashinda dhidi ya Liverpool katika michezo 11, ikifungwa mechi sita na kutoka sare tano, pia haijashinda katika Uwanja wa Anfield kwa miaka mitano.
Mashabiki wanajiuliza ni kwanini Hector Bellerin alichezeshwa sehemu ya beki wa kushoto wakati anachezea mguu wa kulia huku Sead Kolasinac anayechezea mguu wa kushoto kwa asili alikuwepo?
Liverpool ilicheza kwa uelewano mkubwa na kulinda lango lake, ambalo halikuwa na msukosuko mkubwa.
Sehemu ya mlinzi wa kati ilipwaya Aaron Ramsey na Granit Xhaka waliruhusishwa kushambulia lakini wakaacha mlango wazi na kuruhusu washambuliaji wa Liverpool kushambulia.
Kwa upande wa Liverpool, ilikuwa na Jordan Henderson na Georginio Wijnaldum na Emre Can ambao walikuwa wakiwalisha washambuliaji
Roberto Firmino na Sadio Mane walifunga mabao mawili kwa Liverpool kipindi cha kwanza kabla ya Mohamed Salah na Daniel Sturridge kufunga mengine mawili kipindi cha pili.
Kipigo hicho kimefanya Liverpool kufikisha pointi saba katika mechi tatu na kushika nafasi ya pili kwenye msimamo huku Arsenal ikipoteza mchezo wa pili katika mechi tatu. Ilishinda mchezo wa kwanza dhidi ya Leicester City mabao 4-3 kisha ikafungwa bao 1-0.
![]() |
| Mshambuliaji wa Arsenal, Alexis Sanchez akicheka kwa huzuni wakati timu yake ikicheza uwanjani huku ikiwa imepigwa mabao 4-0. |
Katika mechi mbili za mwanzo, Liverpool ilitoka sare ya mabao 3-3 dhidi ya Watford, ilishinda bao 1-0 dhidi ya Crystal Palace.
Liverpool: (4-3-3): Karius,Gomez, Matip, Lovren, Moreno, Wijnaldum, Henderson, Can/Grujic, Mane/Sturridge, Firmino/Milner na Salah.
Arsenal: (3-4-3): Cech , Koscielny, Monreal, Oxlade-Chamberlain/ Lacazette, Xhaka , Ramsey/Coquelin, Bellerin, Sanchez/Giroud , Welbeck na Ozil.
Msimamo Ligi Kuu England
Na Timu P W D L GD PTS1 Manchester United 3 3 0 0 10 9
2 Liverpool 3 2 1 0 5 7
3 Huddersfield Town 3 2 1 0 4 7
4 Manchester City 3 2 1 0 3 7
5 West Brom Albion 3 2 1 0 2 7
6 Chelsea 3 2 0 1 2 6
7 WatfordWatford 3 1 2 0 2 5
8 Southampton 3 1 2 0 1 5
9 Tottenham Hotspur 3 1 1 1 1 4
10 BurnleyBurnley 3 1 1 1 0 4
11 Stoke City 3 1 1 1 0 4
12 EvertonEverton 3 1 1 1 -1 4
13 Swansea City 3 1 1 1 -2 4
14 Newcastle United 3 1 0 2 0 3
15 Leicester City 3 1 0 2 -1 3
16 ArsenalArsenal 3 1 0 2 -4 3
17 Brighton&Hove Albion 3 0 1 2 -4 1
18 Bournemouth 3 0 0 3 -4 0
19 Crystal Palace 3 0 0 3 -6 0
20 West Ham United 3 0 0 3 -8 0



Comments
Post a Comment