Skip to main content

Kanye West, Jay-Z marapa marafiki waliogeuka maadui





Kanye West (kushoto) na Jay-Z

NEW YORK, Marekani
MASHABIKI wa rapa Kanye West wamekerwa na kitendo cha Shawn Corey Carter, maarufu kama Jay-Z kutoa makala ya filamu inayoeleza na kuonesha safari yake ya muziki na wakiwa pamoja kama marafiki kabla ya kutofautiana na kuwa maadui.

Nyota hao ni wasanii waliouza zaidi kazi zao wakiwa na nyimbo nyingi zilizofanya vizuri na wana mamilioni ya mashabiki.

Baada ya kuangalia makala hiyo iliyopewa jina la
Maadui wa Hadharani 'Public Enemies' – Jay-Z vs Kanye iliyorusha na Channel 4 Jumatatu iliyopita, mashabiki  wa Kanye walitumia mtandao wa Twitter kumlaumu rapa wa New York, Jay-Z kwa hatua yake na kusema amemtumia mtu aliyekuwa akimsimamia awali kujikweza kibiashara .

Filamu hiyo iliyopigwa mwaka 2011 imerushwa baada ya nyota hayo waliokuwa rafiki kugeuka maadui na kufanya mashabiki wao kugawanyika.

Baada ya kuonesha uhusiano wao ulivyokuwa katika filamu hiyo, ambapo Jay- Z alikuwa kama mshauri na msimamizi wa msanii mwenzie, mashabiki wa Kanye ambaye ni mzaliwa wa Chicago wameonekana kutofurahia na kumwonea huruma msanii wao.

Filamu hiyo inawaonesha tangu walipokuwa vijana, katika moja ya sehemu anaonekana Eugene McNair (rafiki wa Kanye),  akionesha chumba cha kulala cha Kanye ambacho walikuwa wakitumia kurekodi nyimbo pamoja.

Pia alifungua katika sehemu ya kula, ambayo pia ilikuwa na vifaa vya muziki na vipeperushi vya marapa maarufu, Eugene anaonekana akitoa maelezo ni jinsi gani kazi ya kurekodi ilikuwa ikifanyika wakati huo.

'' Tulikwenda kwenye kitanda chake, alikuwa na mambo yote ya kiafrika katika nyumba, kulikuwa na makasha ya kanda za muziki kila mahali, kulikuwa na picha za utupu, alikuwa na nguo mpya.''

Filamu hiyo haielezi jinsi wawili hao walivyofanyikiwa kuwa juu, lakini inaonesha Jay-Z akiwa na mshauri wa aliyemfanya Kanye kuwa juu.

Baadhi ya watazamaji wamesema prodyuza aliyekuwa kugeuka kuwa rapa, Kanye alikuwa na kipaji zaidi kati yao, huku mtazamaji mmoja akiandika kwenye mtandao: 'Kayne  na Jay-Z,  Jamaa ni jiniasi.'

Tammy Cuff, alisema: 'Ninawapenda wote Jay-Z na Kanye kwa sababu tofauti, lakini College Dropout (albamu ya kwanza ya Kanye)  ilikuwa nzuri na
Jay-Z alikuja kama mtu wa kuwatumia.

Shabiki mmoja, alisema kwamba akiwa kama prodyuza, Kanye alimsaidia Jay-Z kutengeneza nyimbo nzuri zilizofanya vema.

Mwingine alisema Jay -Z anamtumia West kwa biashara zake.

Shabiki wa Jay- Z, Chrome Hitz alimtetea nyota wake kwa kusema kuwa bila ya rapa wa New York, Kanye West asingeweza kupanda juu.

Hata hivyo mashabiki wengine baada ya kuangalia filamu hiyo wameifagilia kwamba imeonesha maisha marapa hao walipitia na wengine kusema wao ni alama ya muziki na wana vipaji vikubwa.

Wawili hao walifanya kazi pamoja 2011, albamu yao ya pamoja 'Watch The Throne' ilifanya vizuri na kuuza nakala nyingi duniani.

Wote wawili wameoa, mbali ya muziki wanajihusisha na biashara ya mavazi.


Jay-Z, ana lebo yake ya muziki ya Roc-A-Fella Records ,  Kanye aliwahi kufanya kazi kwa muda mfupi pamoja naye alipotoka Chicago kwenda New York kutafuta namna ya kutoka.

Baada ya kuacha alifanya muziki kivyake na kuweza kuwa juu katika muziki wa hiphop na kuwa maarufu kama Jay Z.

Albamu nyingine ya Jay-Z inayokuja bado ina alama za vidole vya Kanye ambaye alikuja kuoana na nyota wa runinga, Kim Kardashian.

Kanye kwa sasa haelewani na Jay Z, katika onesho lake alilofanya Sacramento, Marekani alisema amekuwa hampigii simu, anamjua ana watu wanaoweza kupoteza uhai wake (wauaji) lakini asiwatume kumwangamiza.

Pia akiwa jukwaani alimpiga kijembe mke wa Jay-Z, Beyonce kwamba amesikia hafanyi maonesho hadi ashinde tuzo ya video bora ya mwaka na kueleza kuwa hushinda tuzo kwa mipango.

Baada ya kutoa vijembe vyake kwa kutumia kipaza sauti mbele ya mashabiki, Kanye alikitupa jukwaani na kuondoka huku akiwaacha mashabiki wakiwa wamechanganyikiwa.

Kwa wakati huu, Kanye amekuwa akitibiwa ugonjwa wa msongo wa mawazo. Lakini pia kuna habari ameanza kufanya kazi ya kwajili ya kutengeneza albamu yake mpya.

Kwa upande mwingine Jay-Z mwezi uliopita aliachia albamu yake ya  4.44, ambapo kuna wimbo unaonekana kama anaomba radhi kwa Beyonce ambaye hivi karibuni alimzalia watoto pacha kwa kutokuwa mwaminifu kwake.

Comments

Post a Comment

Popular posts from this blog

Wachezaji waliosajiliwa na kuhama timu zote Ligi Kuu England

WAKATI dirisha la usajili Ulaya 2017 lililoanza Juni 9 lNdaniafungwa leo saa sita usiku, ifuatayo ni orodha ya wachezaji walioingia na kutoka katika timu 20 za Ligi Kuu England . Kama wewe ni shabiki wa moja ya timu hizo angalia orodha hii ujue wachezaji walioingia au kuondoka. ARSENAL Ndani Alexandre Lacazette - Lyon (ada haijatajwa), Sead Kolasac - Schalke(bure). Nje Wojciech Szczesny - Juventus, pauni 14m, Gabriel Paulista - Valencia, pauni 10m, Kieran Gibbs - West Brom, pauni 7m, Yaya Sanogo - ameachwa, Stefan O'Connor - ameachwa, Kristopher da Graca - ameachwa,Kostas Pileas - ameachwa, Takuma Asano - Stuttgart- mkopo Chris Willock - Benfica, (ada haijatajwa), Glen Kamara - ameachwa, Marc Bola - Bristol Rovers- mkopo Carl Jenkson - Birmgham- mkopo Cohen Bramall - Birmgham- mkopo Emiliano Martiez - Getafe-mkopo, Stephy Mavididi - Preston-mkopo, Ismael Bennacer - Empoli, (ada haijatajwa), Jon Toral - Hull, (ada haijatajwa). BOURNEMOUTH Ndani Asmir Begovic - Ch...

Zidane ajuta kumtwanga kichwa Materazzi

Picha mbili tofauti zinazomwonesha  Zinedine Zidane alipofanya tukio la kumpiga kichwa Marco Materazzi . MADRID, Hispania KOCHA wa timu ya  Real Madrid Zinedine Zidane amekumbuka tukio alilofanya kwa kumpiga kichwa aliyekuwa mlinzi wa timu ya taifa ya Italia,  Marco Materazzi katika kipindi chake cha mwisho cha uchezaji akisema kuwa hajisikii kujivuna kutokana na tukio hilo. Zidane alifanya tukio hilo wakati akiichezea Real Madrid, wakati akiitumikia Ufaransa katika mechi ya fainali ya kombe la Dunia 2006 ambayo iliisha kwa matokeo ya sare ya bao 1-1 kabla ya Azzuri kushinda kwa mikwaju ya penalti . Zidane ambaye alifanya mahojiano na kituo cha televisheni cha Ufaransa katika kipindi cha Telefoot na kuoneshwa kwenye runinga, alisema anajutia tukio hilo alilofanya katika siku za mwisho kama mchezaji. "Sijisikii kujivunia," Zidane alisema.  Zinedine Zidane akioneshwa kadi nyekundu kutokana na kumpiga kichwa  Marco Materazzi. "Sijivunii tuk...

Wazazi 'wamsusa' mpenzi wa Ronaldo mjamzito

Cristiano Ronaldo akiwa na Georgina Rodriguez na mtoto wao Ronaldo Jr MADRID, Hispania MPENZI wa Cristiano Ronaldo, Georgina Rodriguez anadaiwa kutengwa na wazazi wake. Mrembo huyo mwenye  umri wa miaka 23 anatarajia kujifungua mtoto wa kike Oktoba mwaka huu na kuongeza familia familia yake na Ronaldo inayokuwa kwa  haraka,  lakini kuna taarifa mama na baba yake hawajihusishi katika ujauzito huo. Kwa mujibu wa gazeti la Marca la Hispania, Rodriguez hamekuwan hana uhusiano mzuri na wazazi wake. Limeripoti kuwa kutokana na baba yeke Jorge Eduardo Rodriguez kuishi Argentina, na mama yake, Ana Maria Hernandez yuko nchini Italia, anamaliza kipindi chake cha ujauzito bila ya kupata sapoti. Mwanamitindo huyo mwenye damu mchanganyiko ya Kihispania na ki-Argentina mzaliwa wa Jaca kaskazini mashariki mwa Hispania, amebakia  katika nchi aliyozaliwa na sasa yuko na nyota wa Real Madrid ,anarajia kupata mtoto ambaye atakuwa wa nne kwa Ronaldo. Mtoto atakayemza...