![]() |
| Jafar Iddi (kulia) |
TIMU za Azam na Kagera Sugar zimemaliza mvutano wao kuhusu mvutano wa usajili wa mshambuliaji Mbaraka Yusuf na sasa yuko huru kuichezea.
Baada ya Azam kumtangaza Mbaraka kuwa mmoja wachezaji wake wapya wa msimu huu, ikimpatia mkataba wa miaka miwili, Kagera iliibuka na kusema bado ina mkataba na mchezaji huyo.
Awali Ofisa Habari wa Azam FC, Jaffar Idd, alisema kuwa timu hiyo ilimsajili mchezaji huyo kwa kufuata taratibu zote za usajili, huku akidokeza kuwa tayari Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu(Fifa limeidhinisha usajili wake kupitia mfumo mpya wa usajili wa kimtandao wa TMS.
Pamoja na hilo timu ya Kagara ilipelekea pingamizi TFF ikilalamikia Azam kumsajili nyota huyo.
Hata hivyo Iddi amesema wamemalizana na Kagera Sugar ambao wametoa barua maalum ya kumuachia Mbaraka aitumikie Azam FC.
![]() |
| Mbaraka Yussuf. |


Comments
Post a Comment