Skip to main content

ITC yakwamisha Neymar kucheza leo PSG



PARIS, Ufaransa

NEYMAR ameshindwa kucheza mechi yake ya kwanza katika timu ya Paris Saint-Germain kutokana na kuwepo dosari katika nyaraka za kumwezesha kufanya kazi, zilizotayarishwa na mamlaka za soka za Hispania na Ufaransa.

PSG ilimtambulisha mchezaji huyo ghari zaidi duniani kwa vyombo vya habari Ijumaa iliyopita baada ya kukamilisha uhamisho Alhamisi kwa ada iliyoweka rekodi mpya ya usajili ya pauni 200 (zaidi ya sh. bilioni 589) akitokea Barcelona ya Uhispania, amesaini mkataba wa miaka mitano.

Kiasi cha fedha kilichotumika kama ada ya kumnunua inaweza kununua ndege tatu kubwa za abiria 175 aina ya Boeing 737-700  ambapo kila moja inauzwa  dola milioni 82.4 (zaidi ya sh. bilioni 184.4) kila moja.

Neymar katika utambulisho wake alisema yuko fiti na kuwa tayari kuanza kucheza katika timu ya Parc De Princes katika mchezo wa kwanza wa Ligi Kuu ya Ufaransa  dhidi ya Amien leo.

Hata hivyo, taarifa kutoka Ufaransa zinasema Shirikisho la Mpira wa Miguu Ufaransa, Bodi ya Ligi ilihitaji Hati ya Uhamisho wa Kimataifa (ITC) wa mchezaji huyo Ijumaa ili kumruhusu  acheze mchezo leo jioni.

Hadi kufikia Ijumaa usiku, LFP haikupata nyaraka kutoka  Shirikisho la Mpira wa Miguu la Hispania.

Inafahamika Maofisa wa La Liga  hawajafurahi uhamisho wa wa Neymar huku Rais Javier Tebas akisema shirikisho litatuma malalamiko kwa Shirikisho  la Mpira wa Miguu Ulaya (UEFA) na kudai kuwa klabu ya Ufaransa (PSG) ni ya 'fedha za madawa''.

''Malalamiko tayari na yatawasilishwa kwa UEFA, Umoja wa Ulaya na Mahakama ya Uswisi ,'' alisema Tebas.

'' Kimsingi, malalamiko yanahusu ushindani usiokuwa wa haki na dhidi ya timu ambazo zinaongezewa fedha na wamiliki wake kwa kutoa zawadi ya wachezaji kwa mashabiki wao. PSG ni mfano mzuri wa 'fedha za madawa' aliongeza Tebas.

''Akaunti za PSG zinaonesha kwamba ina mapato makubwa kuliko Real Madrid  au Manchester United,  kitu ambacho kinamaanisha kwamba thamani ya brand yao ni kubwa kuliko klabu hizo mbili . Sawa, hiyo inawezekana,'' alisema

Awali Naymar alitarajia kujumuishwa jana katika mchezo wa kwanza wa Ligi Kuu wa PSG dhidi ya timu ya Amiens ambayo imepanda daraja msimu huu, siku moja tu baada ya kutambulishwa kama mchezaji mpya.

Neymar  amecheza kwa mafanikio misimu minne Nou Camp baada ya kujiunga akitokea  Santos  mwaka  2013 , ametwaa nayo makombe mawili La Liga ,  vikombe vitatu vya Copa del Reys na kimoja cha Ligi ya Mabingwa.

Amejiunga na PSG ambayo katika msimu uliopita ilishika nafasi ya pili katika ligi ikipokwa ubingwa na Monaco,  yenyewe ilitwaa Kombe la Ufaransa na Kombe la Ligi Ufaransa.

Mmiliki wa timu ya PSG, Nasser Al-Khelaifi  amesema melango yake ni kuona wanatwaa taji la Ligi ya Mabingwa baada ya msimu uliopita kutolewa katika hatua ya mtoano ya Ligi ya Mabingwa dhidi ya Barcelona huku Neymar aking'ara kwenye mchezo wa marudiano baada ya kuwa chini kwa mabao manne katika mchezo wa kwanza.

Comments

Popular posts from this blog

Wachezaji waliosajiliwa na kuhama timu zote Ligi Kuu England

WAKATI dirisha la usajili Ulaya 2017 lililoanza Juni 9 lNdaniafungwa leo saa sita usiku, ifuatayo ni orodha ya wachezaji walioingia na kutoka katika timu 20 za Ligi Kuu England . Kama wewe ni shabiki wa moja ya timu hizo angalia orodha hii ujue wachezaji walioingia au kuondoka. ARSENAL Ndani Alexandre Lacazette - Lyon (ada haijatajwa), Sead Kolasac - Schalke(bure). Nje Wojciech Szczesny - Juventus, pauni 14m, Gabriel Paulista - Valencia, pauni 10m, Kieran Gibbs - West Brom, pauni 7m, Yaya Sanogo - ameachwa, Stefan O'Connor - ameachwa, Kristopher da Graca - ameachwa,Kostas Pileas - ameachwa, Takuma Asano - Stuttgart- mkopo Chris Willock - Benfica, (ada haijatajwa), Glen Kamara - ameachwa, Marc Bola - Bristol Rovers- mkopo Carl Jenkson - Birmgham- mkopo Cohen Bramall - Birmgham- mkopo Emiliano Martiez - Getafe-mkopo, Stephy Mavididi - Preston-mkopo, Ismael Bennacer - Empoli, (ada haijatajwa), Jon Toral - Hull, (ada haijatajwa). BOURNEMOUTH Ndani Asmir Begovic - Ch...

Zidane ajuta kumtwanga kichwa Materazzi

Picha mbili tofauti zinazomwonesha  Zinedine Zidane alipofanya tukio la kumpiga kichwa Marco Materazzi . MADRID, Hispania KOCHA wa timu ya  Real Madrid Zinedine Zidane amekumbuka tukio alilofanya kwa kumpiga kichwa aliyekuwa mlinzi wa timu ya taifa ya Italia,  Marco Materazzi katika kipindi chake cha mwisho cha uchezaji akisema kuwa hajisikii kujivuna kutokana na tukio hilo. Zidane alifanya tukio hilo wakati akiichezea Real Madrid, wakati akiitumikia Ufaransa katika mechi ya fainali ya kombe la Dunia 2006 ambayo iliisha kwa matokeo ya sare ya bao 1-1 kabla ya Azzuri kushinda kwa mikwaju ya penalti . Zidane ambaye alifanya mahojiano na kituo cha televisheni cha Ufaransa katika kipindi cha Telefoot na kuoneshwa kwenye runinga, alisema anajutia tukio hilo alilofanya katika siku za mwisho kama mchezaji. "Sijisikii kujivunia," Zidane alisema.  Zinedine Zidane akioneshwa kadi nyekundu kutokana na kumpiga kichwa  Marco Materazzi. "Sijivunii tuk...

Wazazi 'wamsusa' mpenzi wa Ronaldo mjamzito

Cristiano Ronaldo akiwa na Georgina Rodriguez na mtoto wao Ronaldo Jr MADRID, Hispania MPENZI wa Cristiano Ronaldo, Georgina Rodriguez anadaiwa kutengwa na wazazi wake. Mrembo huyo mwenye  umri wa miaka 23 anatarajia kujifungua mtoto wa kike Oktoba mwaka huu na kuongeza familia familia yake na Ronaldo inayokuwa kwa  haraka,  lakini kuna taarifa mama na baba yake hawajihusishi katika ujauzito huo. Kwa mujibu wa gazeti la Marca la Hispania, Rodriguez hamekuwan hana uhusiano mzuri na wazazi wake. Limeripoti kuwa kutokana na baba yeke Jorge Eduardo Rodriguez kuishi Argentina, na mama yake, Ana Maria Hernandez yuko nchini Italia, anamaliza kipindi chake cha ujauzito bila ya kupata sapoti. Mwanamitindo huyo mwenye damu mchanganyiko ya Kihispania na ki-Argentina mzaliwa wa Jaca kaskazini mashariki mwa Hispania, amebakia  katika nchi aliyozaliwa na sasa yuko na nyota wa Real Madrid ,anarajia kupata mtoto ambaye atakuwa wa nne kwa Ronaldo. Mtoto atakayemza...