Skip to main content

Dondoo za usajili Ulaya


Morata kamkimbia Kane Spurs

KOCHA wa Tottenham, Mauricio Pochettino amekiri alifanya mazungumzo na mshambuliaji aliyechukuliwa na Chelsea, Alvaro Morata ajiunge na timu yao , lakini nyota huyo mwenye umri wa miaka 24 hakutaka kugombea namba na Harry Kane. (Daily Mail)

Wenger amkazia Sanchez


KOCHA mhenga wa Arsenal, Arsene Wenger amemwambia kwa maneno makavu mshambuliaji Alexis Sanchez (28), kwamba hatauzwa kwa timu yoyote ya Uingereza katika majira haya ya joto. (Times )


Man U yammendea Aurier

Morata kamkimbia Kane Spurs

KLABU ya Manchester United  inataka kumsiani mlinzi wa kulia wa timu ya Paris St-Germain, Serge Aurier (24), ambaye kwa  sasa ana zuio la kuingia katika nchi za Uingereza.
(Daily Mirror)

Iheanacho huyoo Leicester


MSHAMBULIAJI wa Manchester City raia wa Nigeria, Kelechi Iheanacho (20) hatimaye amepimwa afya katika timu ya Leicester,  ambayo imekubali  kulipa ada ya pauni milioni 25 kwa ajili ya kumsaini.
(Leicester Mercury)

Negredo kutua Besiktas


MSHAMBULIAJI Valencia, Alvaro Negredo (31), anajiandaa kusaini mkataba katika timu ya Besiktas ya Uturuki, pamoja na kutakiwa na timu hasimu za Swansea City na Leeds.
(AS Hispania)

Mahrez 'afosi' kuhasimia Roma



WINGA wa Leicester, Riyad Mahrez (26), yuko tayari kulazimisha uhamisho kwenda Roma,  huku timu yake maarufu kwa jina la mbweha ikisema haiko tayari kumuuza .
(Daily Mirror)

Barca yamtolea macho Dembele


BARCELONA imejiunga kwenye foleni ya kutaka kumsaini mshambuliaji wa Borussia Dortmund , Ousmane Dembele (20), na  wa Juventus Paulo Dybala (23),  kama wa badala wa mchezaji Neymar (25) anayetajwa kutakiwa  na timu ya Paris St-Germain. (Independent)

Comments

Popular posts from this blog

Wachezaji waliosajiliwa na kuhama timu zote Ligi Kuu England

WAKATI dirisha la usajili Ulaya 2017 lililoanza Juni 9 lNdaniafungwa leo saa sita usiku, ifuatayo ni orodha ya wachezaji walioingia na kutoka katika timu 20 za Ligi Kuu England . Kama wewe ni shabiki wa moja ya timu hizo angalia orodha hii ujue wachezaji walioingia au kuondoka. ARSENAL Ndani Alexandre Lacazette - Lyon (ada haijatajwa), Sead Kolasac - Schalke(bure). Nje Wojciech Szczesny - Juventus, pauni 14m, Gabriel Paulista - Valencia, pauni 10m, Kieran Gibbs - West Brom, pauni 7m, Yaya Sanogo - ameachwa, Stefan O'Connor - ameachwa, Kristopher da Graca - ameachwa,Kostas Pileas - ameachwa, Takuma Asano - Stuttgart- mkopo Chris Willock - Benfica, (ada haijatajwa), Glen Kamara - ameachwa, Marc Bola - Bristol Rovers- mkopo Carl Jenkson - Birmgham- mkopo Cohen Bramall - Birmgham- mkopo Emiliano Martiez - Getafe-mkopo, Stephy Mavididi - Preston-mkopo, Ismael Bennacer - Empoli, (ada haijatajwa), Jon Toral - Hull, (ada haijatajwa). BOURNEMOUTH Ndani Asmir Begovic - Ch...

Zidane ajuta kumtwanga kichwa Materazzi

Picha mbili tofauti zinazomwonesha  Zinedine Zidane alipofanya tukio la kumpiga kichwa Marco Materazzi . MADRID, Hispania KOCHA wa timu ya  Real Madrid Zinedine Zidane amekumbuka tukio alilofanya kwa kumpiga kichwa aliyekuwa mlinzi wa timu ya taifa ya Italia,  Marco Materazzi katika kipindi chake cha mwisho cha uchezaji akisema kuwa hajisikii kujivuna kutokana na tukio hilo. Zidane alifanya tukio hilo wakati akiichezea Real Madrid, wakati akiitumikia Ufaransa katika mechi ya fainali ya kombe la Dunia 2006 ambayo iliisha kwa matokeo ya sare ya bao 1-1 kabla ya Azzuri kushinda kwa mikwaju ya penalti . Zidane ambaye alifanya mahojiano na kituo cha televisheni cha Ufaransa katika kipindi cha Telefoot na kuoneshwa kwenye runinga, alisema anajutia tukio hilo alilofanya katika siku za mwisho kama mchezaji. "Sijisikii kujivunia," Zidane alisema.  Zinedine Zidane akioneshwa kadi nyekundu kutokana na kumpiga kichwa  Marco Materazzi. "Sijivunii tuk...

Wazazi 'wamsusa' mpenzi wa Ronaldo mjamzito

Cristiano Ronaldo akiwa na Georgina Rodriguez na mtoto wao Ronaldo Jr MADRID, Hispania MPENZI wa Cristiano Ronaldo, Georgina Rodriguez anadaiwa kutengwa na wazazi wake. Mrembo huyo mwenye  umri wa miaka 23 anatarajia kujifungua mtoto wa kike Oktoba mwaka huu na kuongeza familia familia yake na Ronaldo inayokuwa kwa  haraka,  lakini kuna taarifa mama na baba yake hawajihusishi katika ujauzito huo. Kwa mujibu wa gazeti la Marca la Hispania, Rodriguez hamekuwan hana uhusiano mzuri na wazazi wake. Limeripoti kuwa kutokana na baba yeke Jorge Eduardo Rodriguez kuishi Argentina, na mama yake, Ana Maria Hernandez yuko nchini Italia, anamaliza kipindi chake cha ujauzito bila ya kupata sapoti. Mwanamitindo huyo mwenye damu mchanganyiko ya Kihispania na ki-Argentina mzaliwa wa Jaca kaskazini mashariki mwa Hispania, amebakia  katika nchi aliyozaliwa na sasa yuko na nyota wa Real Madrid ,anarajia kupata mtoto ambaye atakuwa wa nne kwa Ronaldo. Mtoto atakayemza...