Morata kamkimbia Kane Spurs
KOCHA wa Tottenham, Mauricio Pochettino amekiri alifanya mazungumzo na mshambuliaji aliyechukuliwa na Chelsea, Alvaro Morata ajiunge na timu yao , lakini nyota huyo mwenye umri wa miaka 24 hakutaka kugombea namba na Harry Kane. (Daily Mail)
Wenger amkazia Sanchez
KOCHA mhenga wa Arsenal, Arsene Wenger amemwambia kwa maneno makavu mshambuliaji Alexis Sanchez (28), kwamba hatauzwa kwa timu yoyote ya Uingereza katika majira haya ya joto. (Times )
Man U yammendea Aurier
Morata kamkimbia Kane Spurs
KLABU ya Manchester United inataka kumsiani mlinzi wa kulia wa timu ya Paris St-Germain, Serge Aurier (24), ambaye kwa sasa ana zuio la kuingia katika nchi za Uingereza.
(Daily Mirror)
Iheanacho huyoo Leicester
MSHAMBULIAJI wa Manchester City raia wa Nigeria, Kelechi Iheanacho (20) hatimaye amepimwa afya katika timu ya Leicester, ambayo imekubali kulipa ada ya pauni milioni 25 kwa ajili ya kumsaini.
(Leicester Mercury)
Negredo kutua Besiktas
MSHAMBULIAJI Valencia, Alvaro Negredo (31), anajiandaa kusaini mkataba katika timu ya Besiktas ya Uturuki, pamoja na kutakiwa na timu hasimu za Swansea City na Leeds.
(AS Hispania)
Mahrez 'afosi' kuhasimia Roma
WINGA wa Leicester, Riyad Mahrez (26), yuko tayari kulazimisha uhamisho kwenda Roma, huku timu yake maarufu kwa jina la mbweha ikisema haiko tayari kumuuza .
(Daily Mirror)
Barca yamtolea macho Dembele
BARCELONA imejiunga kwenye foleni ya kutaka kumsaini mshambuliaji wa Borussia Dortmund , Ousmane Dembele (20), na wa Juventus Paulo Dybala (23), kama wa badala wa mchezaji Neymar (25) anayetajwa kutakiwa na timu ya Paris St-Germain. (Independent)







Comments
Post a Comment