Skip to main content

Diamond , Harmonize, Mavoko, Rayvanny washambulia katika Zilipendwa


Nassibu Abdul maarufu kama Diamond Platnumz (wapili kushoto) na wasanii wenzie wanavyoonekana katika Video ya wimbo wa Zilipendwa uliopakuliwa leo.

Mwandishi wetu

WASANII wa Kundi la Wasafi Classic Baby (WBC), Diamond Mlatnumz, Harmonize, Rich Mavoko, Maromboso, Queen Darleen, Lavalava na Rayvanny wametoa video ya wimbo wao mpya uitwao Zilipendwa ambao wameimba mambo mbalimbali ya zamani (mambo ya wahenga).

Katika wimbo huo ambao tayari umeanza kupigwa kwenye vituo vya televisheni, redio na kwenye mitandao ya kijamii, wameimba na kufanya ulinganifu wa mambo zamani na sasa sasa wakiangalia kuhusu mapenzi, ugomvi na kutokuelewana kwa watu kulikobakia kama simulizi au zilipendwa.

Wimbo huo umetoka siku moja tu baada ya kutoka wimbo wa msanii Ali Kiba wa Seduce Me (Nitongoze mimi) kitu ambacho kimefanya mashabiki wa pande zote mbili kushindana  kwa kupishana kila upande ukiutambia mwingine kuwa wimbo wao ni mzuri.

Katika video Diamond na wasanii wenzie wanaonekana wamekiwa wamevaa mavazi ya zamani na kutumia ala za muziki wamewatumia wasanii waigizaji, kuendana namaneno yanayoimbwa kwenye wimbo huo.




Mapenzi ya zamani zamani wanatu walikuwa wakipelekeana kadi na maua mtu anaridhika , mtu kusema kuwa anampenda mwingine hadi kumwona kwenye glasi ya maji lakini kwa wanwake wa leo wanataka mikakati, ukiwa mzugaji huwapati.

Kuhusu mambo ya zamani waliyoyaimba kama ni zilipendwa ni kama kupiga chabo (kuchungulia ndani kupitia dirishani) na kutaja orodha watu walikuwa na uhusiano wa kimapenzi na kuachana ambapo katika kuonesha kuwa hawabagui pia ametajwa Diamond na Wema.

Kuhusu watu waliokuwa na hasama ambao wamebaki kama zilizopengwa wametajwa wengi ikiwemo, Bashite na Gwajima, pia mitindo ya muziki ya zamani kama bolingo, ndombolo, Chipolopolo, Simba wa Morogoro ( Afande Sele), MB Dog wa Latifah, Babu Tale Papa Misifa na hata pati watu hawaendi kibisa imebaki zilipendwa.

Mpira na Pele zilipendwa, Dandu na Nyerere, Asha ngedere, Arous Mabele, Idi Amini, masuala ya kuuza nyumba ili kuweka heshima baa nayo pia  zilipendwa.

Mwishoni mwa wimbo huo wanaweza hata masualaya madili yaliyokuwepo enzi za Rais Kikwete sasa enzi za Magufuli imekuwa zilipendwa!

Comments

Popular posts from this blog

Wachezaji waliosajiliwa na kuhama timu zote Ligi Kuu England

WAKATI dirisha la usajili Ulaya 2017 lililoanza Juni 9 lNdaniafungwa leo saa sita usiku, ifuatayo ni orodha ya wachezaji walioingia na kutoka katika timu 20 za Ligi Kuu England . Kama wewe ni shabiki wa moja ya timu hizo angalia orodha hii ujue wachezaji walioingia au kuondoka. ARSENAL Ndani Alexandre Lacazette - Lyon (ada haijatajwa), Sead Kolasac - Schalke(bure). Nje Wojciech Szczesny - Juventus, pauni 14m, Gabriel Paulista - Valencia, pauni 10m, Kieran Gibbs - West Brom, pauni 7m, Yaya Sanogo - ameachwa, Stefan O'Connor - ameachwa, Kristopher da Graca - ameachwa,Kostas Pileas - ameachwa, Takuma Asano - Stuttgart- mkopo Chris Willock - Benfica, (ada haijatajwa), Glen Kamara - ameachwa, Marc Bola - Bristol Rovers- mkopo Carl Jenkson - Birmgham- mkopo Cohen Bramall - Birmgham- mkopo Emiliano Martiez - Getafe-mkopo, Stephy Mavididi - Preston-mkopo, Ismael Bennacer - Empoli, (ada haijatajwa), Jon Toral - Hull, (ada haijatajwa). BOURNEMOUTH Ndani Asmir Begovic - Ch...

Zidane ajuta kumtwanga kichwa Materazzi

Picha mbili tofauti zinazomwonesha  Zinedine Zidane alipofanya tukio la kumpiga kichwa Marco Materazzi . MADRID, Hispania KOCHA wa timu ya  Real Madrid Zinedine Zidane amekumbuka tukio alilofanya kwa kumpiga kichwa aliyekuwa mlinzi wa timu ya taifa ya Italia,  Marco Materazzi katika kipindi chake cha mwisho cha uchezaji akisema kuwa hajisikii kujivuna kutokana na tukio hilo. Zidane alifanya tukio hilo wakati akiichezea Real Madrid, wakati akiitumikia Ufaransa katika mechi ya fainali ya kombe la Dunia 2006 ambayo iliisha kwa matokeo ya sare ya bao 1-1 kabla ya Azzuri kushinda kwa mikwaju ya penalti . Zidane ambaye alifanya mahojiano na kituo cha televisheni cha Ufaransa katika kipindi cha Telefoot na kuoneshwa kwenye runinga, alisema anajutia tukio hilo alilofanya katika siku za mwisho kama mchezaji. "Sijisikii kujivunia," Zidane alisema.  Zinedine Zidane akioneshwa kadi nyekundu kutokana na kumpiga kichwa  Marco Materazzi. "Sijivunii tuk...

Wazazi 'wamsusa' mpenzi wa Ronaldo mjamzito

Cristiano Ronaldo akiwa na Georgina Rodriguez na mtoto wao Ronaldo Jr MADRID, Hispania MPENZI wa Cristiano Ronaldo, Georgina Rodriguez anadaiwa kutengwa na wazazi wake. Mrembo huyo mwenye  umri wa miaka 23 anatarajia kujifungua mtoto wa kike Oktoba mwaka huu na kuongeza familia familia yake na Ronaldo inayokuwa kwa  haraka,  lakini kuna taarifa mama na baba yake hawajihusishi katika ujauzito huo. Kwa mujibu wa gazeti la Marca la Hispania, Rodriguez hamekuwan hana uhusiano mzuri na wazazi wake. Limeripoti kuwa kutokana na baba yeke Jorge Eduardo Rodriguez kuishi Argentina, na mama yake, Ana Maria Hernandez yuko nchini Italia, anamaliza kipindi chake cha ujauzito bila ya kupata sapoti. Mwanamitindo huyo mwenye damu mchanganyiko ya Kihispania na ki-Argentina mzaliwa wa Jaca kaskazini mashariki mwa Hispania, amebakia  katika nchi aliyozaliwa na sasa yuko na nyota wa Real Madrid ,anarajia kupata mtoto ambaye atakuwa wa nne kwa Ronaldo. Mtoto atakayemza...