Skip to main content

Dembele apimwa afya Barcelona


Ousmane Dembele akipimwa afya katika timu ya Barcelona leo.
 LONDON, Uingereza
KIUNGO Ousmane Dembele amepimwa afya na kuonekana kuwa fiti  kabla ya kusaini mkataba wa miaka mitano wa pauni milioni 96 (zaidi ya sh. bilioni 277.5) Barcelona.
Nyota huyo wa  Ufaransa  mwenye umri wa miaka 20, atatarajiwa kutambulishwa kwa mashabiki Jumatatu, baada ya kusaini mkataba wa miaka mitano kwa miamba ya Catalan.
Nyota huyo aliwasili kwenye kituo cha mazoezi cha klabu Ciutat Esportiva leo asubuhi, na kufanyiwa vipimo akihamia timu hiyo akitokea Borussia Dortmund.
Katika video iliyoachiwa na Barcelona kupitia mtandao wake wa twitter, inamwonesha akifanya mazoezi kwenye gym akiwa ni sehemu ya vipimo vya ufiti wa mwili. 
Uje ya Uwanja wa Nou Camp, kulikuwa na mashabiki wengi waliofika kutaka kuona wakati akitambulishwa.
Dembele kwa sasa ni ni mchezaji wa pili ghari zaidi akiwa nyuma ya  nyota wa Brazil, Neymar aliyesainiwa na PSG kwa ada ya pauni milioni 200 (zaidi ya sh. bilioni 578).
''Nina furaha sana hapa.  Imekuwa ni ndoto yangu kila wakati kuwa katika Barcelona, Dembele alisema na kukaririwa na tovuti ya klabu baada ya kusaini mkataba wa miaka mitano. 
Inaaminika dili ya kuleta Dembele Uwanja wa Nou Camp itaigharimu Barcelona hadi kufikia pauni 136 (zaidi ya sh. bilioni 393). 
Mshambuliaji huyo ameachwa kwenye kikosi cha ufaransa kwa ajili mechi mbili zijazo za kuwania kufuzu fainali za Kombe la Dunia dhidi ya Uholanzi na Luxembourg baada ya kutofanya mazoezi katika iliyokuwa timu yake Dortmund  wakati akijiandaa kwa uhamisho huo.

Comments

Popular posts from this blog

Wachezaji waliosajiliwa na kuhama timu zote Ligi Kuu England

WAKATI dirisha la usajili Ulaya 2017 lililoanza Juni 9 lNdaniafungwa leo saa sita usiku, ifuatayo ni orodha ya wachezaji walioingia na kutoka katika timu 20 za Ligi Kuu England . Kama wewe ni shabiki wa moja ya timu hizo angalia orodha hii ujue wachezaji walioingia au kuondoka. ARSENAL Ndani Alexandre Lacazette - Lyon (ada haijatajwa), Sead Kolasac - Schalke(bure). Nje Wojciech Szczesny - Juventus, pauni 14m, Gabriel Paulista - Valencia, pauni 10m, Kieran Gibbs - West Brom, pauni 7m, Yaya Sanogo - ameachwa, Stefan O'Connor - ameachwa, Kristopher da Graca - ameachwa,Kostas Pileas - ameachwa, Takuma Asano - Stuttgart- mkopo Chris Willock - Benfica, (ada haijatajwa), Glen Kamara - ameachwa, Marc Bola - Bristol Rovers- mkopo Carl Jenkson - Birmgham- mkopo Cohen Bramall - Birmgham- mkopo Emiliano Martiez - Getafe-mkopo, Stephy Mavididi - Preston-mkopo, Ismael Bennacer - Empoli, (ada haijatajwa), Jon Toral - Hull, (ada haijatajwa). BOURNEMOUTH Ndani Asmir Begovic - Ch...

Zidane ajuta kumtwanga kichwa Materazzi

Picha mbili tofauti zinazomwonesha  Zinedine Zidane alipofanya tukio la kumpiga kichwa Marco Materazzi . MADRID, Hispania KOCHA wa timu ya  Real Madrid Zinedine Zidane amekumbuka tukio alilofanya kwa kumpiga kichwa aliyekuwa mlinzi wa timu ya taifa ya Italia,  Marco Materazzi katika kipindi chake cha mwisho cha uchezaji akisema kuwa hajisikii kujivuna kutokana na tukio hilo. Zidane alifanya tukio hilo wakati akiichezea Real Madrid, wakati akiitumikia Ufaransa katika mechi ya fainali ya kombe la Dunia 2006 ambayo iliisha kwa matokeo ya sare ya bao 1-1 kabla ya Azzuri kushinda kwa mikwaju ya penalti . Zidane ambaye alifanya mahojiano na kituo cha televisheni cha Ufaransa katika kipindi cha Telefoot na kuoneshwa kwenye runinga, alisema anajutia tukio hilo alilofanya katika siku za mwisho kama mchezaji. "Sijisikii kujivunia," Zidane alisema.  Zinedine Zidane akioneshwa kadi nyekundu kutokana na kumpiga kichwa  Marco Materazzi. "Sijivunii tuk...

Wazazi 'wamsusa' mpenzi wa Ronaldo mjamzito

Cristiano Ronaldo akiwa na Georgina Rodriguez na mtoto wao Ronaldo Jr MADRID, Hispania MPENZI wa Cristiano Ronaldo, Georgina Rodriguez anadaiwa kutengwa na wazazi wake. Mrembo huyo mwenye  umri wa miaka 23 anatarajia kujifungua mtoto wa kike Oktoba mwaka huu na kuongeza familia familia yake na Ronaldo inayokuwa kwa  haraka,  lakini kuna taarifa mama na baba yake hawajihusishi katika ujauzito huo. Kwa mujibu wa gazeti la Marca la Hispania, Rodriguez hamekuwan hana uhusiano mzuri na wazazi wake. Limeripoti kuwa kutokana na baba yeke Jorge Eduardo Rodriguez kuishi Argentina, na mama yake, Ana Maria Hernandez yuko nchini Italia, anamaliza kipindi chake cha ujauzito bila ya kupata sapoti. Mwanamitindo huyo mwenye damu mchanganyiko ya Kihispania na ki-Argentina mzaliwa wa Jaca kaskazini mashariki mwa Hispania, amebakia  katika nchi aliyozaliwa na sasa yuko na nyota wa Real Madrid ,anarajia kupata mtoto ambaye atakuwa wa nne kwa Ronaldo. Mtoto atakayemza...