Mwandishi wetu
BARAZA la Mpira wa Miguu kwa Nchi za Kusini mwa Afrika (Cosafa), limetoa zawadi ya dola 10,000 (zaidi ya sh milioni 22) kwa Taifa Stars ya Tanzania ikiwa ni zawadi kwa kuwa mshindi wa tatu katika mashindano yake yaliofanyika mwezi uliopita nchini Afrika Kusini.
Katika taarifa ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) iliyotolewa leo na Ofisa habari wake, Alfred Lucas wameamua fedha hizo zitolewe kwa wachezaji wote walioshiriki fainali hizo pamoja na benchi la ufundi.
Lucas alisema pia Cosafa imetuma fedha za zawadi kwa wachezaji wa Tanzania ambao walifanya vema kwenye mashindano hayo .
Wachezaji hao ni Shiza Kichuya aliyekuwa Mchezaji Bora katika mechi kati ya Tanzania na Malawi; Mzamiru Yassin aliyeibuka Mchezaji Bora wa mechi kati ya Tanzania na Angola; Erasto Nyoni aliyeibuka Mchezaji Bora wa mechi kati ya Tanzania na Mauritius; Elius Maguri aliyeibuka Mchezaji Bora wa mechi kati ya Tanzania na Afrika Kusini huku Kipa Bora wa michuano hiyo ni Said Mohammed .
Tanzania iliifunga Lesotho na kushika nafasi ya tatu.

Comments
Post a Comment