Skip to main content

Chelsea yaacha wachezaji 26, yabaki na 17





LONDON, Uingereza

HUKU ikiwa zimesalia siku 10 kabla ya kuanza kwa Ligi Kuu England msimu wa 2017/18 kikosi cha kwanza cha Mabingwa watetezi wa Chelsea kina wachezaji 17 tu.

Chelsea hivi karibuni imemuuza mlinzi wake Nemanja Matic kwa mahasimu wao Manchester United, hali inayokiacha kikosi kikiwa na huzuni  huku kukiwa na muda mfupi kabla ya Ligi Kuu na Ligi ya Mabingwa kuanza .

Katika msimu huu  Chelsea imemsaini Alvaro Morata kwa ada ya pauni milioni 70.6 (zaidi ya sh. bilioni 209), Tiemoue Bakayoko kwa pauni milioni 40 (zaidi ya sh. bil 118), Antonio Rudiger  kwa ada ya pauni milioni 31 zaidi ya sh. bil 91) na Willy Caballero  bure

Ikijumuishwa wachezaji iliyowatoa kwa mkopo, Chelsea  katika majira haya ya joyo imewaachia wachezaji 26 wakiwemo Nathan Ake, Kurt Zouma, Asmir Begovic, Diego Costa na Matic.

Wadau wa woka wanalaumu kwa kitendo chake cha kukubali kumuuza Matic kwa Manchester United ambao ni hasimu wao.

Kocha Antonio Conte amekuwa akilalamika kwa kutosapotiwa na uongozi kusajili wachezaji wapya wakati timu inakabiliwa na mashindano mbalimbali.


Hata hivyo Chelsea  bado iko sokoni  ikisaka wachezaji.

Inamwinda Alex Sandro wa Juventus na Antonio Candreva wa Inter wachezaji ambao wamependekezwa na Conte.

Pia inadaiwa kumwinda  kiungo wa Leicester,  Danny Drinkwater na Alexis Sanches wa Arsenal ambaye leo ameungana na wachezaji wenzie kwenye mazoezi baada ya kutoka katika mapumziko, nyota huyo atajajwa pia kutakiwa na Bayern.

Comments

Popular posts from this blog

Wachezaji waliosajiliwa na kuhama timu zote Ligi Kuu England

WAKATI dirisha la usajili Ulaya 2017 lililoanza Juni 9 lNdaniafungwa leo saa sita usiku, ifuatayo ni orodha ya wachezaji walioingia na kutoka katika timu 20 za Ligi Kuu England . Kama wewe ni shabiki wa moja ya timu hizo angalia orodha hii ujue wachezaji walioingia au kuondoka. ARSENAL Ndani Alexandre Lacazette - Lyon (ada haijatajwa), Sead Kolasac - Schalke(bure). Nje Wojciech Szczesny - Juventus, pauni 14m, Gabriel Paulista - Valencia, pauni 10m, Kieran Gibbs - West Brom, pauni 7m, Yaya Sanogo - ameachwa, Stefan O'Connor - ameachwa, Kristopher da Graca - ameachwa,Kostas Pileas - ameachwa, Takuma Asano - Stuttgart- mkopo Chris Willock - Benfica, (ada haijatajwa), Glen Kamara - ameachwa, Marc Bola - Bristol Rovers- mkopo Carl Jenkson - Birmgham- mkopo Cohen Bramall - Birmgham- mkopo Emiliano Martiez - Getafe-mkopo, Stephy Mavididi - Preston-mkopo, Ismael Bennacer - Empoli, (ada haijatajwa), Jon Toral - Hull, (ada haijatajwa). BOURNEMOUTH Ndani Asmir Begovic - Ch...

Zidane ajuta kumtwanga kichwa Materazzi

Picha mbili tofauti zinazomwonesha  Zinedine Zidane alipofanya tukio la kumpiga kichwa Marco Materazzi . MADRID, Hispania KOCHA wa timu ya  Real Madrid Zinedine Zidane amekumbuka tukio alilofanya kwa kumpiga kichwa aliyekuwa mlinzi wa timu ya taifa ya Italia,  Marco Materazzi katika kipindi chake cha mwisho cha uchezaji akisema kuwa hajisikii kujivuna kutokana na tukio hilo. Zidane alifanya tukio hilo wakati akiichezea Real Madrid, wakati akiitumikia Ufaransa katika mechi ya fainali ya kombe la Dunia 2006 ambayo iliisha kwa matokeo ya sare ya bao 1-1 kabla ya Azzuri kushinda kwa mikwaju ya penalti . Zidane ambaye alifanya mahojiano na kituo cha televisheni cha Ufaransa katika kipindi cha Telefoot na kuoneshwa kwenye runinga, alisema anajutia tukio hilo alilofanya katika siku za mwisho kama mchezaji. "Sijisikii kujivunia," Zidane alisema.  Zinedine Zidane akioneshwa kadi nyekundu kutokana na kumpiga kichwa  Marco Materazzi. "Sijivunii tuk...

Wazazi 'wamsusa' mpenzi wa Ronaldo mjamzito

Cristiano Ronaldo akiwa na Georgina Rodriguez na mtoto wao Ronaldo Jr MADRID, Hispania MPENZI wa Cristiano Ronaldo, Georgina Rodriguez anadaiwa kutengwa na wazazi wake. Mrembo huyo mwenye  umri wa miaka 23 anatarajia kujifungua mtoto wa kike Oktoba mwaka huu na kuongeza familia familia yake na Ronaldo inayokuwa kwa  haraka,  lakini kuna taarifa mama na baba yake hawajihusishi katika ujauzito huo. Kwa mujibu wa gazeti la Marca la Hispania, Rodriguez hamekuwan hana uhusiano mzuri na wazazi wake. Limeripoti kuwa kutokana na baba yeke Jorge Eduardo Rodriguez kuishi Argentina, na mama yake, Ana Maria Hernandez yuko nchini Italia, anamaliza kipindi chake cha ujauzito bila ya kupata sapoti. Mwanamitindo huyo mwenye damu mchanganyiko ya Kihispania na ki-Argentina mzaliwa wa Jaca kaskazini mashariki mwa Hispania, amebakia  katika nchi aliyozaliwa na sasa yuko na nyota wa Real Madrid ,anarajia kupata mtoto ambaye atakuwa wa nne kwa Ronaldo. Mtoto atakayemza...