Skip to main content

Cheka aikatia rufaa adhabu ya TPBC



Cosmas Cheka akizungumza na waandishi wa habari Dar es salaam jana kuhusu kuchukua ya kukata rufaa Baraza la Michezo la Taifa (BMT), kupinga kufungiwa na matokeo ya pambano lake dhidi ya bondia Haidary Mchanjo. Kulia ni meneja wake, Juma Ndambile.

Mwandishi Wetu
BONDIA wa ngumi za kulipwa nchini, Cosmas Cheka amekata rufaa Baraza la Michezo la Taifa (BMT) kupinga matokeo, adhabu ya kufungiwa miezi sita na faini ya Sh. 200,000 iliyotangazwa na Kamisheni ya Ngumi za Kulipwa Tanzania (TPBC).
Cheka alisema hayo jana kwenye mkutano na waandishi wa habari na kusema  TPBC ilikuwa na njama dhidi yake ili kumtengenezea nafasi bondia Haidary Mchanjo katika ngumi za kulipwa nchini.
Alifafanua, adhabu dhidi yake haikufuata sheria kwani kwanza hakupewa nafasi ya kusikilizwa kwa mujibu wa sheria, huku TPBC ikimpa nafasi mwamuzi wa pambano hilo, Modest Rashid  aliyetaka kupigana naye kujieleza katika kikao cha TPBC.
“Hata kwenye mahakama, lazima mtuhumiwa apewe nafasi ya kusikilizwa au kujitetea, mimi nilikuwa ulingoni na mwamuzi na mpinzani wangu Mchanjo, mwamuzi amenitolea maneno machafu sana, haikutosha akaamua kunikata pointi, niliandika barua ya kulalamika TPBC, hawajaniita na kuibuka na adhabu kwangu,” alisema Cheka.
Alisema kuwa pamoja na uamuzi huo kutomfikia kimaandishi, ameamua kuchukua hatua za haraka kwani tayari vyombo vya habari mbalimbali na mitandao ya kijamii vimekwishatangaza uamuzi uliofanywa bila kufuata sheria kwa kumpa nafasi ya kumsikiliza.

Meneja wa bondia huyo, Juma Ndambile, alisema  walichokifanya TPBC ni kumvunja nguvu bondia wake ili ashindwe kuendelea na mchezo wake.
 “Niliwaambia kuwa pambano limeandaliwa na kampuni inayoitwa Dragon, sasa kwa nini mimi nilipe, pia niliambiwa nitafute hela ya glovu, niligoma, nadhani hiyo ndiyo imekuwa chanzo,” alisema Ndambile.
Alisema  ili kumpata mshindi sahihi, bora pambano hilo lilirudiwe ili mshindi apatikane kwa mujibu wa taratibu na siyo kwa njia iliyotumika ambayo lengo lake ni kuharibu rekodi na kutengeneza ya bondia mwingine.

Awali juzi TPBC ilitangaza kumfungia Cheka kwa kufanya fujo baada ya pambano lililofanyika ukumbi wa Vijana Kinondoni kati yake na Mchanjo ambaye alitangazwa kuwa mshindi.

Comments

Popular posts from this blog

Wachezaji waliosajiliwa na kuhama timu zote Ligi Kuu England

WAKATI dirisha la usajili Ulaya 2017 lililoanza Juni 9 lNdaniafungwa leo saa sita usiku, ifuatayo ni orodha ya wachezaji walioingia na kutoka katika timu 20 za Ligi Kuu England . Kama wewe ni shabiki wa moja ya timu hizo angalia orodha hii ujue wachezaji walioingia au kuondoka. ARSENAL Ndani Alexandre Lacazette - Lyon (ada haijatajwa), Sead Kolasac - Schalke(bure). Nje Wojciech Szczesny - Juventus, pauni 14m, Gabriel Paulista - Valencia, pauni 10m, Kieran Gibbs - West Brom, pauni 7m, Yaya Sanogo - ameachwa, Stefan O'Connor - ameachwa, Kristopher da Graca - ameachwa,Kostas Pileas - ameachwa, Takuma Asano - Stuttgart- mkopo Chris Willock - Benfica, (ada haijatajwa), Glen Kamara - ameachwa, Marc Bola - Bristol Rovers- mkopo Carl Jenkson - Birmgham- mkopo Cohen Bramall - Birmgham- mkopo Emiliano Martiez - Getafe-mkopo, Stephy Mavididi - Preston-mkopo, Ismael Bennacer - Empoli, (ada haijatajwa), Jon Toral - Hull, (ada haijatajwa). BOURNEMOUTH Ndani Asmir Begovic - Ch...

Zidane ajuta kumtwanga kichwa Materazzi

Picha mbili tofauti zinazomwonesha  Zinedine Zidane alipofanya tukio la kumpiga kichwa Marco Materazzi . MADRID, Hispania KOCHA wa timu ya  Real Madrid Zinedine Zidane amekumbuka tukio alilofanya kwa kumpiga kichwa aliyekuwa mlinzi wa timu ya taifa ya Italia,  Marco Materazzi katika kipindi chake cha mwisho cha uchezaji akisema kuwa hajisikii kujivuna kutokana na tukio hilo. Zidane alifanya tukio hilo wakati akiichezea Real Madrid, wakati akiitumikia Ufaransa katika mechi ya fainali ya kombe la Dunia 2006 ambayo iliisha kwa matokeo ya sare ya bao 1-1 kabla ya Azzuri kushinda kwa mikwaju ya penalti . Zidane ambaye alifanya mahojiano na kituo cha televisheni cha Ufaransa katika kipindi cha Telefoot na kuoneshwa kwenye runinga, alisema anajutia tukio hilo alilofanya katika siku za mwisho kama mchezaji. "Sijisikii kujivunia," Zidane alisema.  Zinedine Zidane akioneshwa kadi nyekundu kutokana na kumpiga kichwa  Marco Materazzi. "Sijivunii tuk...

Wazazi 'wamsusa' mpenzi wa Ronaldo mjamzito

Cristiano Ronaldo akiwa na Georgina Rodriguez na mtoto wao Ronaldo Jr MADRID, Hispania MPENZI wa Cristiano Ronaldo, Georgina Rodriguez anadaiwa kutengwa na wazazi wake. Mrembo huyo mwenye  umri wa miaka 23 anatarajia kujifungua mtoto wa kike Oktoba mwaka huu na kuongeza familia familia yake na Ronaldo inayokuwa kwa  haraka,  lakini kuna taarifa mama na baba yake hawajihusishi katika ujauzito huo. Kwa mujibu wa gazeti la Marca la Hispania, Rodriguez hamekuwan hana uhusiano mzuri na wazazi wake. Limeripoti kuwa kutokana na baba yeke Jorge Eduardo Rodriguez kuishi Argentina, na mama yake, Ana Maria Hernandez yuko nchini Italia, anamaliza kipindi chake cha ujauzito bila ya kupata sapoti. Mwanamitindo huyo mwenye damu mchanganyiko ya Kihispania na ki-Argentina mzaliwa wa Jaca kaskazini mashariki mwa Hispania, amebakia  katika nchi aliyozaliwa na sasa yuko na nyota wa Real Madrid ,anarajia kupata mtoto ambaye atakuwa wa nne kwa Ronaldo. Mtoto atakayemza...