Skip to main content

Bolt bado awaza kucheza soka Man Utd


Usain Bolt

USAIN Bolt anaamini kuwa anaweza kupata timu ya kuchezea baada ya kustaafu mchezo wa riadha.

Kwa sasa inawezekana  anajiandaa kukubali ofa ya kujiunga na timu ya League One au League Two kuliko timu anayoipenda ya Manchester United.

Boltn (30) ametangaza kujiuzulu kushirikishi mashindano ya riadha baada ya kutwaa medali 19, huku akipata medali ya shaba moja katika  mbio za meta 100 za mashindano ya Dunia ya London yalioisha mwishoni mwa wiki.

Nyota huyo wa Jamaica, hakuweza kumaliza mbio za relay 4x100m Jumamosi kutokana na kushikwa na msuli na amesema: “kila wakati zilikuwa nikitaka kucheza soka kwa sababu ni kitu ninachofikiria , nimekuwa mzuri katika  hicho.

“Lakini kwa sasa baada kuumia msuli, nimekuwa sina mashaka makubwa sana kuhusu hilo kwa sasa.”

Wakala wa Bolt, Ricky Simms ameliambia gazeti la Daily Star kwam,ba anataka kucheza soka na kwamba wana ofa za klabu nyingi zinazotaka aende kufanya majaribio.

“Sitaki kutaja majina lakini atakwenda Dortmund kwa kuwa CEO (Ofisa Mtendaji Mkuu wa Puma, ambaye ni rafiki yetu yumo kwenye bodi ya Borussia Dortmund. Atakwenda kufanya mazoezi nao .

“Mwanariadha huyo mwenye umri wa miaka 30 anaweza kucheza katika Bundesliga au Premier League? Kiukweli ni hatua ya mbali zaidi.

“Ninafikiri kama atapata muda wa miezi sita au tisa ya kufanya mzopezi na kucheza mechi za kirafiki na timu anaweza kucheza kwa daraja fulani hiyo inaweza kuwa katika League One au League Two.”

Kabla ya hiyo yote, Bolt anatumaini kuwa fiti na kucheza katika mechi kati ya wachezaji nyota wa zamani wa United dhidi ya Barcelona  katika Uwanja wa Old Trafford, Septemba 2, mwaka huu.

Katika mechi hiyo ndipo anaweza kuonesha ni kwa kiasi gani mzuri uwanjani.

 Simms aliongeza “ anaweza kunipiga mimi kichwani na kusema kuwa anakwenda kucheza katika Ligi ya Mabingwa.

“Lakini sijui kikweli kama amehamasika katika hatua hii ya maisha yake kwenda kufanya mazoezi na wachezaji wa akiba katika siku ya mvua Manchester au Munich au sehemu nyingine kwa kuwa ni mtu mwenye fedha na maisha mazuri. Mnaweza kumuona kupiti katika soka.”

Mchezaji aliyenunuliwa kwa dau kubwa United, Paul Pogba awali alisema kwamba anatarajia Bolt anasaini katika timu ya Jose Mourinho inayosaka ubingwa msimu huu.

Comments

Popular posts from this blog

Wachezaji waliosajiliwa na kuhama timu zote Ligi Kuu England

WAKATI dirisha la usajili Ulaya 2017 lililoanza Juni 9 lNdaniafungwa leo saa sita usiku, ifuatayo ni orodha ya wachezaji walioingia na kutoka katika timu 20 za Ligi Kuu England . Kama wewe ni shabiki wa moja ya timu hizo angalia orodha hii ujue wachezaji walioingia au kuondoka. ARSENAL Ndani Alexandre Lacazette - Lyon (ada haijatajwa), Sead Kolasac - Schalke(bure). Nje Wojciech Szczesny - Juventus, pauni 14m, Gabriel Paulista - Valencia, pauni 10m, Kieran Gibbs - West Brom, pauni 7m, Yaya Sanogo - ameachwa, Stefan O'Connor - ameachwa, Kristopher da Graca - ameachwa,Kostas Pileas - ameachwa, Takuma Asano - Stuttgart- mkopo Chris Willock - Benfica, (ada haijatajwa), Glen Kamara - ameachwa, Marc Bola - Bristol Rovers- mkopo Carl Jenkson - Birmgham- mkopo Cohen Bramall - Birmgham- mkopo Emiliano Martiez - Getafe-mkopo, Stephy Mavididi - Preston-mkopo, Ismael Bennacer - Empoli, (ada haijatajwa), Jon Toral - Hull, (ada haijatajwa). BOURNEMOUTH Ndani Asmir Begovic - Ch...

Zidane ajuta kumtwanga kichwa Materazzi

Picha mbili tofauti zinazomwonesha  Zinedine Zidane alipofanya tukio la kumpiga kichwa Marco Materazzi . MADRID, Hispania KOCHA wa timu ya  Real Madrid Zinedine Zidane amekumbuka tukio alilofanya kwa kumpiga kichwa aliyekuwa mlinzi wa timu ya taifa ya Italia,  Marco Materazzi katika kipindi chake cha mwisho cha uchezaji akisema kuwa hajisikii kujivuna kutokana na tukio hilo. Zidane alifanya tukio hilo wakati akiichezea Real Madrid, wakati akiitumikia Ufaransa katika mechi ya fainali ya kombe la Dunia 2006 ambayo iliisha kwa matokeo ya sare ya bao 1-1 kabla ya Azzuri kushinda kwa mikwaju ya penalti . Zidane ambaye alifanya mahojiano na kituo cha televisheni cha Ufaransa katika kipindi cha Telefoot na kuoneshwa kwenye runinga, alisema anajutia tukio hilo alilofanya katika siku za mwisho kama mchezaji. "Sijisikii kujivunia," Zidane alisema.  Zinedine Zidane akioneshwa kadi nyekundu kutokana na kumpiga kichwa  Marco Materazzi. "Sijivunii tuk...

Wazazi 'wamsusa' mpenzi wa Ronaldo mjamzito

Cristiano Ronaldo akiwa na Georgina Rodriguez na mtoto wao Ronaldo Jr MADRID, Hispania MPENZI wa Cristiano Ronaldo, Georgina Rodriguez anadaiwa kutengwa na wazazi wake. Mrembo huyo mwenye  umri wa miaka 23 anatarajia kujifungua mtoto wa kike Oktoba mwaka huu na kuongeza familia familia yake na Ronaldo inayokuwa kwa  haraka,  lakini kuna taarifa mama na baba yake hawajihusishi katika ujauzito huo. Kwa mujibu wa gazeti la Marca la Hispania, Rodriguez hamekuwan hana uhusiano mzuri na wazazi wake. Limeripoti kuwa kutokana na baba yeke Jorge Eduardo Rodriguez kuishi Argentina, na mama yake, Ana Maria Hernandez yuko nchini Italia, anamaliza kipindi chake cha ujauzito bila ya kupata sapoti. Mwanamitindo huyo mwenye damu mchanganyiko ya Kihispania na ki-Argentina mzaliwa wa Jaca kaskazini mashariki mwa Hispania, amebakia  katika nchi aliyozaliwa na sasa yuko na nyota wa Real Madrid ,anarajia kupata mtoto ambaye atakuwa wa nne kwa Ronaldo. Mtoto atakayemza...