Skip to main content

Bolt akana starehe kumwangusha London

Bolt akiwa na mpenzi wake, Kasi Bennett


MWANARIADHA Usain Bolt alifanya starehe usiku kucha kabla ya kukimbia mbio za mwisho za relay 4x100 ambazo alishindwa kumaliza kwa kushikwa na msuli katika mguu wa kushoto.

Rafiki wa karibu aliyekuwa naye katika kujirusha, alisema Bolt alipokuwa klabu usiku alichangamka kwa kucheza na kunywa  huku akisalimia kila mtu alikuwa naye karibu, alikuwa kivutio kwa watu waliokuwepo klabu hasa akina dada.

Alisema alimwona akimbusu mdada mmoja alikwepo kwenye klabu hiyo, alijirusha hadi saa 12 asubuhi siku ya mashindano.

Alisema alipokuwa klabu alikuwa akinywa wiski aina ya Hennessy na Wray na Nephew ambzo zote za kijamaica.

Bolt na wenzie walikumbuka maisha ya rafiki yake wa tangu utotoni nchini,Germaine Mason aliyekuwa akishiriki mchezo wa kuruka juu, aliyetwaa medali ya fedha kwa timu ya Uingereza mwaka 2008.

Mason alifariki kwa ajali wakati akiendesha baiskeli, akitoka kwenye hafla nchini jamaica, Aprili mwaka huu.

Akiwa na rafiki zake alishiriki kuchimba kaburi  na kubeba jeneza, pia alikwenda kuona sehemu alipopatia ajali.

Bolti anasema kifo cha ghafla cha Mason ikiwa na umri wa kiaka  34 kimemwathiri sana, hakufanya mazoezi ya kutosha kutokana na tukio hilo.

Bolt alisema baada ya mazishi ya rafiki yake hakuweza kufanya mazoezi kwa wiki mbili au mbili na nusu, aliamua kupumzika ili kujiweka sawa.

Alisema mwaka huu umekuwa mgumu kwake, alikuwa na mtazamo wa kutaka kushinda na kuwafurahisha mashabiki wake lakini haikuwa hivyo.

Matumaini ya Bolt kustaafu riadha vizuri kwa ushindi katika mbio za meta 100 yalitowekwa kujikuta akishinda nafasi ya tatu na kupata medali ya shaba akiwa, nyuma ya Mmarekani Justin Gatlin ambaye aliwahi kufungiwa kwa kashfa ya kutumia dawa za kusisimua misuli na Christian Coleman akishika nafasi ya pili.

Bolti amekanusha kwamba kushindwa kwake kufanya vizuri kumechangiwa na kufanya kwake starehe kwenye klabu za usiku London.

Bolt bingwa mara tisa wa medali za dhahabu katika Olimpiki na rafiki zake walionekana katika eneo la VIP la The Box Soho, akiwa na watu maarufu kuna wakati alitembelewa na Prince Harry.

Comments

Popular posts from this blog

Wachezaji waliosajiliwa na kuhama timu zote Ligi Kuu England

WAKATI dirisha la usajili Ulaya 2017 lililoanza Juni 9 lNdaniafungwa leo saa sita usiku, ifuatayo ni orodha ya wachezaji walioingia na kutoka katika timu 20 za Ligi Kuu England . Kama wewe ni shabiki wa moja ya timu hizo angalia orodha hii ujue wachezaji walioingia au kuondoka. ARSENAL Ndani Alexandre Lacazette - Lyon (ada haijatajwa), Sead Kolasac - Schalke(bure). Nje Wojciech Szczesny - Juventus, pauni 14m, Gabriel Paulista - Valencia, pauni 10m, Kieran Gibbs - West Brom, pauni 7m, Yaya Sanogo - ameachwa, Stefan O'Connor - ameachwa, Kristopher da Graca - ameachwa,Kostas Pileas - ameachwa, Takuma Asano - Stuttgart- mkopo Chris Willock - Benfica, (ada haijatajwa), Glen Kamara - ameachwa, Marc Bola - Bristol Rovers- mkopo Carl Jenkson - Birmgham- mkopo Cohen Bramall - Birmgham- mkopo Emiliano Martiez - Getafe-mkopo, Stephy Mavididi - Preston-mkopo, Ismael Bennacer - Empoli, (ada haijatajwa), Jon Toral - Hull, (ada haijatajwa). BOURNEMOUTH Ndani Asmir Begovic - Ch...

Zidane ajuta kumtwanga kichwa Materazzi

Picha mbili tofauti zinazomwonesha  Zinedine Zidane alipofanya tukio la kumpiga kichwa Marco Materazzi . MADRID, Hispania KOCHA wa timu ya  Real Madrid Zinedine Zidane amekumbuka tukio alilofanya kwa kumpiga kichwa aliyekuwa mlinzi wa timu ya taifa ya Italia,  Marco Materazzi katika kipindi chake cha mwisho cha uchezaji akisema kuwa hajisikii kujivuna kutokana na tukio hilo. Zidane alifanya tukio hilo wakati akiichezea Real Madrid, wakati akiitumikia Ufaransa katika mechi ya fainali ya kombe la Dunia 2006 ambayo iliisha kwa matokeo ya sare ya bao 1-1 kabla ya Azzuri kushinda kwa mikwaju ya penalti . Zidane ambaye alifanya mahojiano na kituo cha televisheni cha Ufaransa katika kipindi cha Telefoot na kuoneshwa kwenye runinga, alisema anajutia tukio hilo alilofanya katika siku za mwisho kama mchezaji. "Sijisikii kujivunia," Zidane alisema.  Zinedine Zidane akioneshwa kadi nyekundu kutokana na kumpiga kichwa  Marco Materazzi. "Sijivunii tuk...

Wazazi 'wamsusa' mpenzi wa Ronaldo mjamzito

Cristiano Ronaldo akiwa na Georgina Rodriguez na mtoto wao Ronaldo Jr MADRID, Hispania MPENZI wa Cristiano Ronaldo, Georgina Rodriguez anadaiwa kutengwa na wazazi wake. Mrembo huyo mwenye  umri wa miaka 23 anatarajia kujifungua mtoto wa kike Oktoba mwaka huu na kuongeza familia familia yake na Ronaldo inayokuwa kwa  haraka,  lakini kuna taarifa mama na baba yake hawajihusishi katika ujauzito huo. Kwa mujibu wa gazeti la Marca la Hispania, Rodriguez hamekuwan hana uhusiano mzuri na wazazi wake. Limeripoti kuwa kutokana na baba yeke Jorge Eduardo Rodriguez kuishi Argentina, na mama yake, Ana Maria Hernandez yuko nchini Italia, anamaliza kipindi chake cha ujauzito bila ya kupata sapoti. Mwanamitindo huyo mwenye damu mchanganyiko ya Kihispania na ki-Argentina mzaliwa wa Jaca kaskazini mashariki mwa Hispania, amebakia  katika nchi aliyozaliwa na sasa yuko na nyota wa Real Madrid ,anarajia kupata mtoto ambaye atakuwa wa nne kwa Ronaldo. Mtoto atakayemza...