Skip to main content

Bodi ya Ligi yaiangukia Yanga




Boniface Wambura


Mwandishi wetu

WAKATI uongozi wa Yanga ukiitaka Bodi ya Ligi Tanzania (TPLB) kuwaomba radhi  kutokana na kutowatumia mwaliko katika hafla ya kukabidhi vifaa kwa timu 16 zinazoshiriki Ligi Kuu, bodi hiyo imefanya hivyo.

Ofisa Habari wa Yanga, Dismas Ten alisema jana walishindwa kwenda katika hafla ya utoaji vifaa kwa kuwa hawakupata mwaliko  kutoka TFF na Bodi ya Ligi.

''Yanga mbali ya kuwa klabu kubwa pia ni mabinga watetezi wa Ligi ya Vodacom, ilipaswa kutumia mwaliko mapema na si siku moja kabla ya tukio.''

Akizungumzia tukio hilo jana , Mtendaji Mkuu wa Bondi ya Ligi, Boniface Wambura alisema wanaomba radhi kutokana na kuchelewa kupeleka mwaliko kwa njia ya mtandao.

Kiungweana tunaitaka radhi Yanga, ingawa hata viongozi wengine waliofika kwenye hafala ya kukabidhi vifaa walikuja baada ya kuona mwaliako kwenye mtandao, njia ambayo tumekuwa tukiitumia mara kwa mara.


Katika hafla ya utoaji jezi iliyofanyika jana Dar es Salaam,  Yanga haikuwa na mwakilishi, kitu kilichoifanya  Ofisa Habari wa  Simba, Haji Manara kujiokeza kupokea jezi kwa niaba yao, huku akipiga kijembe  kuwa wamekuwa na tabia ya kuchelewa chelewa katika matukio.

Wakati akitoa kijembe hicho Simba nayo haikutokea katika hafla ya kukabidhi zawadi wa washindi wa Ligi Kuu ya Vodadom 2016-17.

Simba ilishika nafasi ya pili nyuma ya Yanga iliyotwaa ubingwa kwa tofauti ya mabao ya kufunga. Pia Mchezaji Bora wa ligi alitoka kweny klabu yao, Mohammed Hussein 'Tshabalala'.

Comments

Popular posts from this blog

Wachezaji waliosajiliwa na kuhama timu zote Ligi Kuu England

WAKATI dirisha la usajili Ulaya 2017 lililoanza Juni 9 lNdaniafungwa leo saa sita usiku, ifuatayo ni orodha ya wachezaji walioingia na kutoka katika timu 20 za Ligi Kuu England . Kama wewe ni shabiki wa moja ya timu hizo angalia orodha hii ujue wachezaji walioingia au kuondoka. ARSENAL Ndani Alexandre Lacazette - Lyon (ada haijatajwa), Sead Kolasac - Schalke(bure). Nje Wojciech Szczesny - Juventus, pauni 14m, Gabriel Paulista - Valencia, pauni 10m, Kieran Gibbs - West Brom, pauni 7m, Yaya Sanogo - ameachwa, Stefan O'Connor - ameachwa, Kristopher da Graca - ameachwa,Kostas Pileas - ameachwa, Takuma Asano - Stuttgart- mkopo Chris Willock - Benfica, (ada haijatajwa), Glen Kamara - ameachwa, Marc Bola - Bristol Rovers- mkopo Carl Jenkson - Birmgham- mkopo Cohen Bramall - Birmgham- mkopo Emiliano Martiez - Getafe-mkopo, Stephy Mavididi - Preston-mkopo, Ismael Bennacer - Empoli, (ada haijatajwa), Jon Toral - Hull, (ada haijatajwa). BOURNEMOUTH Ndani Asmir Begovic - Ch...

Zidane ajuta kumtwanga kichwa Materazzi

Picha mbili tofauti zinazomwonesha  Zinedine Zidane alipofanya tukio la kumpiga kichwa Marco Materazzi . MADRID, Hispania KOCHA wa timu ya  Real Madrid Zinedine Zidane amekumbuka tukio alilofanya kwa kumpiga kichwa aliyekuwa mlinzi wa timu ya taifa ya Italia,  Marco Materazzi katika kipindi chake cha mwisho cha uchezaji akisema kuwa hajisikii kujivuna kutokana na tukio hilo. Zidane alifanya tukio hilo wakati akiichezea Real Madrid, wakati akiitumikia Ufaransa katika mechi ya fainali ya kombe la Dunia 2006 ambayo iliisha kwa matokeo ya sare ya bao 1-1 kabla ya Azzuri kushinda kwa mikwaju ya penalti . Zidane ambaye alifanya mahojiano na kituo cha televisheni cha Ufaransa katika kipindi cha Telefoot na kuoneshwa kwenye runinga, alisema anajutia tukio hilo alilofanya katika siku za mwisho kama mchezaji. "Sijisikii kujivunia," Zidane alisema.  Zinedine Zidane akioneshwa kadi nyekundu kutokana na kumpiga kichwa  Marco Materazzi. "Sijivunii tuk...

Wazazi 'wamsusa' mpenzi wa Ronaldo mjamzito

Cristiano Ronaldo akiwa na Georgina Rodriguez na mtoto wao Ronaldo Jr MADRID, Hispania MPENZI wa Cristiano Ronaldo, Georgina Rodriguez anadaiwa kutengwa na wazazi wake. Mrembo huyo mwenye  umri wa miaka 23 anatarajia kujifungua mtoto wa kike Oktoba mwaka huu na kuongeza familia familia yake na Ronaldo inayokuwa kwa  haraka,  lakini kuna taarifa mama na baba yake hawajihusishi katika ujauzito huo. Kwa mujibu wa gazeti la Marca la Hispania, Rodriguez hamekuwan hana uhusiano mzuri na wazazi wake. Limeripoti kuwa kutokana na baba yeke Jorge Eduardo Rodriguez kuishi Argentina, na mama yake, Ana Maria Hernandez yuko nchini Italia, anamaliza kipindi chake cha ujauzito bila ya kupata sapoti. Mwanamitindo huyo mwenye damu mchanganyiko ya Kihispania na ki-Argentina mzaliwa wa Jaca kaskazini mashariki mwa Hispania, amebakia  katika nchi aliyozaliwa na sasa yuko na nyota wa Real Madrid ,anarajia kupata mtoto ambaye atakuwa wa nne kwa Ronaldo. Mtoto atakayemza...