Skip to main content

Barca, Madrid zaanza kwa ushindi La Liga



Gareth Bale akimruka mlindamlango  Deportivo, Ruben Martinez.

TIMU za Barcelona na Real Madrid zimeibuka na ushindi katika michezo yao ya kwanza ya La Liga msimu huu dhidi ya timu za Real Betis na Deportivo La Coruna.

Barcelona ilishinda mabao 2-0 dhidi ya Real Betis 2-0 katika uwanja wa Nou Camp,ukiwa ni mchezo wao wa kwanza tangu kutokea mashambulio ya kutisha la kigaidi katika mji mkuu wa Catalan na Cambrils.

Real Madrid imeanza kampeni yake ya kutetea ubingwa kwa mara ya kwanza tangu mwaka 2008 kwa ushindi wa mabao 3-0 ugenini dhidi ya Deportivo La Coruna, huku Sergio Ramos akitolewa kwa kadi nyekundu katika sekunde za mwisho.

Mlinzi wa Betis, Alin Tosca alijifunga wakati akiwa kwenye jitihaza za kuokoa mpira wa krosi kutoka kwa Gerard Deulofeu wa Barcelona dakika ya 36, huku mshambuliaji wa zamani wa Everton aliyerusi katika timu yake aliyoichezea utotoni pia alitoa pasi ya bao la pili kwa
Sergi Roberto dakika ya 39.

Wachezaji wa Barcelona wakipongezana baada ya kupata bao

Katika mchezo huo, Lionel Messi alikuwa na mzigo mzito wa kuongoza safu ya ushambuliaji kutokana na kutowepo Luis Suarez  na Andres Iniesta, hakufunga bao lakini aligongesha mwamba mara  tatu.

Gareth Bale alifunga bao la kwanza kwa Madrid dakika ya 20 kabla ya Casemiro kuongeza la pili  dakika saba kabla ya filimbi ya mwisho .

Toni Kroos  kisha alikutana mpira kutoka kwa Bale na kufunga bao la tatu kwa Real dakika ya  62 , kabla ya Ramos kuoneshwa kadi ya pili ya njano katika muda wa majeruhi.

Comments

Popular posts from this blog

Wachezaji waliosajiliwa na kuhama timu zote Ligi Kuu England

WAKATI dirisha la usajili Ulaya 2017 lililoanza Juni 9 lNdaniafungwa leo saa sita usiku, ifuatayo ni orodha ya wachezaji walioingia na kutoka katika timu 20 za Ligi Kuu England . Kama wewe ni shabiki wa moja ya timu hizo angalia orodha hii ujue wachezaji walioingia au kuondoka. ARSENAL Ndani Alexandre Lacazette - Lyon (ada haijatajwa), Sead Kolasac - Schalke(bure). Nje Wojciech Szczesny - Juventus, pauni 14m, Gabriel Paulista - Valencia, pauni 10m, Kieran Gibbs - West Brom, pauni 7m, Yaya Sanogo - ameachwa, Stefan O'Connor - ameachwa, Kristopher da Graca - ameachwa,Kostas Pileas - ameachwa, Takuma Asano - Stuttgart- mkopo Chris Willock - Benfica, (ada haijatajwa), Glen Kamara - ameachwa, Marc Bola - Bristol Rovers- mkopo Carl Jenkson - Birmgham- mkopo Cohen Bramall - Birmgham- mkopo Emiliano Martiez - Getafe-mkopo, Stephy Mavididi - Preston-mkopo, Ismael Bennacer - Empoli, (ada haijatajwa), Jon Toral - Hull, (ada haijatajwa). BOURNEMOUTH Ndani Asmir Begovic - Ch...

Zidane ajuta kumtwanga kichwa Materazzi

Picha mbili tofauti zinazomwonesha  Zinedine Zidane alipofanya tukio la kumpiga kichwa Marco Materazzi . MADRID, Hispania KOCHA wa timu ya  Real Madrid Zinedine Zidane amekumbuka tukio alilofanya kwa kumpiga kichwa aliyekuwa mlinzi wa timu ya taifa ya Italia,  Marco Materazzi katika kipindi chake cha mwisho cha uchezaji akisema kuwa hajisikii kujivuna kutokana na tukio hilo. Zidane alifanya tukio hilo wakati akiichezea Real Madrid, wakati akiitumikia Ufaransa katika mechi ya fainali ya kombe la Dunia 2006 ambayo iliisha kwa matokeo ya sare ya bao 1-1 kabla ya Azzuri kushinda kwa mikwaju ya penalti . Zidane ambaye alifanya mahojiano na kituo cha televisheni cha Ufaransa katika kipindi cha Telefoot na kuoneshwa kwenye runinga, alisema anajutia tukio hilo alilofanya katika siku za mwisho kama mchezaji. "Sijisikii kujivunia," Zidane alisema.  Zinedine Zidane akioneshwa kadi nyekundu kutokana na kumpiga kichwa  Marco Materazzi. "Sijivunii tuk...

Wazazi 'wamsusa' mpenzi wa Ronaldo mjamzito

Cristiano Ronaldo akiwa na Georgina Rodriguez na mtoto wao Ronaldo Jr MADRID, Hispania MPENZI wa Cristiano Ronaldo, Georgina Rodriguez anadaiwa kutengwa na wazazi wake. Mrembo huyo mwenye  umri wa miaka 23 anatarajia kujifungua mtoto wa kike Oktoba mwaka huu na kuongeza familia familia yake na Ronaldo inayokuwa kwa  haraka,  lakini kuna taarifa mama na baba yake hawajihusishi katika ujauzito huo. Kwa mujibu wa gazeti la Marca la Hispania, Rodriguez hamekuwan hana uhusiano mzuri na wazazi wake. Limeripoti kuwa kutokana na baba yeke Jorge Eduardo Rodriguez kuishi Argentina, na mama yake, Ana Maria Hernandez yuko nchini Italia, anamaliza kipindi chake cha ujauzito bila ya kupata sapoti. Mwanamitindo huyo mwenye damu mchanganyiko ya Kihispania na ki-Argentina mzaliwa wa Jaca kaskazini mashariki mwa Hispania, amebakia  katika nchi aliyozaliwa na sasa yuko na nyota wa Real Madrid ,anarajia kupata mtoto ambaye atakuwa wa nne kwa Ronaldo. Mtoto atakayemza...