Skip to main content

Ada ya Neymar inanunua ndege za Boeing tatu!




PARIS, Ufaransa

TIMU ya Paris St-Germain imekamilisha dili la kumnunua mshambuliaji wa Brazil, Neymar, kwa ada iliyoweka rekodi mpya ya usajili ya pauni 200 (zaidi ya sh. bilioni 589) akitokea timu ya  Barcelona.

Ada hiyo iliyotumiaka kumnunua Neymar inaweza kununua ndege tatu kubwa za abiria aina ya Boeing 737-700  ambapo kila moja inauzwa  dola milioni 82.4 (zaidi ya sh. bilioni 184.4) kila moja.

Ada ya nyota huyo mwenye umri wa miaka 25 imevunja rekodi ya awali iliyowekwa Paul Pogba alipotua Manchester United kutoka Juventus kwa pauni milioni 89 (zaidi ya sh. bilioni 261) Agosti 2016.

Katika mkataba wake atakuwa akilipwa pauni milioni 40.7 (zaidi ya kwa mwaka sh. bilioni 119) kwa mwaka akipata mshahara wa pauni 782,000 (zaidi ya sh. bilioni 2.3) kila wiki, malipo hayo ni kabla ya  kulipa kodi katika mkataba wake wa miaka mitano.

Akizungumza baada ya kusaini mkataba Neymar alisema amefurahi kujiunga na moja ya timu kubwa Ulaya".

"Nilikuwa na ndoto kubwa ya kujiunga na Paris St-Germain, pamoja na kujitoleza kwao na nguvu zinazotokana na hili," alisema.

"Najihisi niko tayari kuanza kazi. Kuanzia leo, nitafanya kila niwezalo kuwasaidia wachezaji wenzangu wapya."

Neymar  atatambulishwa rasmi kwa mashabiki wa PSG kesho  wakati wa mechi yao ya kwanza kabisa ya msimu mpya, ambayo itakuwa nyumbani uwanja wa Parc des Princes dhidi ya Amiens.


Nchini Uhispania, kifungu cha kumwachilia mchezaji kutoka kwa mkataba wake kinaweza tu kufunguliwa kwa mchezaji kulipa pesa yeye binafsi.

Neymar alipofika na pesa Alhamisi kulipa hata hivyo, maafisa wa La Liga walikataa malipo hayo.

Awali  kulitokea majibizano kati ya maofisa wa La Liga na wasimamizi wa Ligue 1.
La Liga wanaamini PSG huenda wanakiuka sheria za uchezaji haki kifedha (FFP) kwa kumnunua mchezaji huyo wa Brazil.

Baada ya kushindwa kulipa pesa hizo kwa La Liga, wawakilishi wa Neymar walilipa pauni milioni 200 katika ofisi ya Ofisi za Barcelona FC.

Neymar alijiunga na Barca mwaka 2013 na  kushinda nayo mataji mawili ya La Liga na moja la Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya.

Aliichezea Barcelona mechi yake ya kwanza dhidi ya Levante Agosti 2013, amefungia mabao 105 na kusaidia ufungaji wa mengine 80 katika mechi 186 .

Alichezea timu ya taifa ya Brazil mara ya kwanza akiwa na miaka18 na kufunga mabao 52 katika mechi 77.

Comments

Popular posts from this blog

Wachezaji waliosajiliwa na kuhama timu zote Ligi Kuu England

WAKATI dirisha la usajili Ulaya 2017 lililoanza Juni 9 lNdaniafungwa leo saa sita usiku, ifuatayo ni orodha ya wachezaji walioingia na kutoka katika timu 20 za Ligi Kuu England . Kama wewe ni shabiki wa moja ya timu hizo angalia orodha hii ujue wachezaji walioingia au kuondoka. ARSENAL Ndani Alexandre Lacazette - Lyon (ada haijatajwa), Sead Kolasac - Schalke(bure). Nje Wojciech Szczesny - Juventus, pauni 14m, Gabriel Paulista - Valencia, pauni 10m, Kieran Gibbs - West Brom, pauni 7m, Yaya Sanogo - ameachwa, Stefan O'Connor - ameachwa, Kristopher da Graca - ameachwa,Kostas Pileas - ameachwa, Takuma Asano - Stuttgart- mkopo Chris Willock - Benfica, (ada haijatajwa), Glen Kamara - ameachwa, Marc Bola - Bristol Rovers- mkopo Carl Jenkson - Birmgham- mkopo Cohen Bramall - Birmgham- mkopo Emiliano Martiez - Getafe-mkopo, Stephy Mavididi - Preston-mkopo, Ismael Bennacer - Empoli, (ada haijatajwa), Jon Toral - Hull, (ada haijatajwa). BOURNEMOUTH Ndani Asmir Begovic - Ch...

Zidane ajuta kumtwanga kichwa Materazzi

Picha mbili tofauti zinazomwonesha  Zinedine Zidane alipofanya tukio la kumpiga kichwa Marco Materazzi . MADRID, Hispania KOCHA wa timu ya  Real Madrid Zinedine Zidane amekumbuka tukio alilofanya kwa kumpiga kichwa aliyekuwa mlinzi wa timu ya taifa ya Italia,  Marco Materazzi katika kipindi chake cha mwisho cha uchezaji akisema kuwa hajisikii kujivuna kutokana na tukio hilo. Zidane alifanya tukio hilo wakati akiichezea Real Madrid, wakati akiitumikia Ufaransa katika mechi ya fainali ya kombe la Dunia 2006 ambayo iliisha kwa matokeo ya sare ya bao 1-1 kabla ya Azzuri kushinda kwa mikwaju ya penalti . Zidane ambaye alifanya mahojiano na kituo cha televisheni cha Ufaransa katika kipindi cha Telefoot na kuoneshwa kwenye runinga, alisema anajutia tukio hilo alilofanya katika siku za mwisho kama mchezaji. "Sijisikii kujivunia," Zidane alisema.  Zinedine Zidane akioneshwa kadi nyekundu kutokana na kumpiga kichwa  Marco Materazzi. "Sijivunii tuk...

Wazazi 'wamsusa' mpenzi wa Ronaldo mjamzito

Cristiano Ronaldo akiwa na Georgina Rodriguez na mtoto wao Ronaldo Jr MADRID, Hispania MPENZI wa Cristiano Ronaldo, Georgina Rodriguez anadaiwa kutengwa na wazazi wake. Mrembo huyo mwenye  umri wa miaka 23 anatarajia kujifungua mtoto wa kike Oktoba mwaka huu na kuongeza familia familia yake na Ronaldo inayokuwa kwa  haraka,  lakini kuna taarifa mama na baba yake hawajihusishi katika ujauzito huo. Kwa mujibu wa gazeti la Marca la Hispania, Rodriguez hamekuwan hana uhusiano mzuri na wazazi wake. Limeripoti kuwa kutokana na baba yeke Jorge Eduardo Rodriguez kuishi Argentina, na mama yake, Ana Maria Hernandez yuko nchini Italia, anamaliza kipindi chake cha ujauzito bila ya kupata sapoti. Mwanamitindo huyo mwenye damu mchanganyiko ya Kihispania na ki-Argentina mzaliwa wa Jaca kaskazini mashariki mwa Hispania, amebakia  katika nchi aliyozaliwa na sasa yuko na nyota wa Real Madrid ,anarajia kupata mtoto ambaye atakuwa wa nne kwa Ronaldo. Mtoto atakayemza...