![]() |
| Justi Gatlin akiwa amepiga magoti kuonesha kwa heshima kwa Usain Bolt baada ya kumshinda katika mbio za meta 100 leo. |
MWANARIADHA aliyekuwa
akitajwa kuwa na kasi zaidi duniani, Usain Bolt ameshindwa kutetea
ubingwa wake wa Dunia katika mbio meta 100, akibwagwa na hasimu wake, Mmarekani Justin Gatlin katika mashindano ya yanayoendelea
London, Uingereza.
Awali
Bolt alitangazakuwa atatarajia kustaafu
riadha, kwa kupotea taji hilo ina maana anamaliza vibaya.
Katika
fainali ya mbio zilizofanyika leo, Bolt ameshika nafasi ya tatu, huku mpinzani wake, Gatlin aliyekuwa
akimponda kwa kufungiwa mara mbili kwa kutumi dawa za kusisimua misuli akiibuka
na ushindi.
Awali
katika Bolt ingawa alishinda hakumaliza kwa muda mzuri akitumia zaidi ya
sekunde 10, katika mbio za leo hakuanza vizuri kwa kasi pia hata umaliziaji
wake.
Mwisho
Gatlin aliyekuwa nyuma akaongeza kasi na kumpita na Mmarekani mwingine,
Christian Coleman akampita na kushika nafasi ya pili.
Hata
hivyo, mashabiki waliendelea kumuaga Bolt kwa shangwe kubwa katika shindano
lake hilo la mwisho.
Bolt
sasa amebakiza mbio za relai 4x100 (za
kupokezana vijiti) ambazo pia anashikilia ubingwa atakazokibia JUmatano baada
ya hapo anatarajiwa kustaafu.

Comments
Post a Comment